WAREMBO wanaotarajiwa kushiriki shindano la Miss Higher
Learning 2013 wataanza mazoezi rasmi
Ijumaa ya Juni 21, mazoezi yatakayofanyika kwenye hoteli ya Grand Villa iliyopo
Kijitonyama, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Aggy Classic Entertainment inayoandaa shindano hilo Aggness Mathew
alisema kwamba warembo hao watanolewa na mrembo aliyepata kutwaa taji la Kanda
hiyo mwaka 2010, Blessing Ngowi (pichani).
“Mpaka sasa ni wadhamini wakuu wa Miss Tanzania kinywaji cha Redd’s
Original ndio wamethibitisha kudhamini, hivyo tunaomba wadhamini wengine
kujitokeza kudhamini shindano letu,”alisema
Comments
Post a Comment