WAKATI aliyekuwa kocha wa Simba Mfaransa Patrick Liewig akitua nchini jana na
kudai hatambui kutimuliwa kwake kazi, uongozi wa Simba umesema kocha huyo ni
muongo kwani tayari alishakabidhiwa barua.
Simba ilimtimua kukatisha mkataba wa mwaka mmoja wa kazi wa
kocha huyo baada ya kutoridhishwa na utendaji wake baada ya kumalizika kwa
msimu uliopita wa ligi kuu bara na timu kuishia nafasi ya tatu.
Akizungumza jijini jana, Liewing alisema anatambua bado ana
mkataba na wekundu hao wa Msimbazi unamalizika hadi mwezi juni hivyo amerejea kuendelea na kibarua chake
baada ya mapumziko mafupi.
Alisema wakati anaondoka uongozi haukumpa taarifa kama
unaachana naye na ndiyo maana aliacha vitu vyake katika hoteli aliyokuwa
akiishi na kama wangemwambia ukweli angecxhukua kila kilicho chake.
Hata hivyo, Liewig alikiri kufahamu kuwa nafasi yake kwa
sasa imechukuliwa na kocha mwingine na kuongeza kuwa baada ya kulifahamu hilo
alizungumza na mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage ambaye alimuahidi kuonana naye ili kutatua
tatizo lake.
“Kama kweli wameamua kuachana na mimi ni bora wanilipe
changu ili tuachane vizuri kwani sitaki matatizo na mtu, hivyo nasubiri kuonana
na mwenyeki (Rage) kama tulivyokubaliana na baada ya hapo nitajua nini hatima
yangu,”alisema Liewig
Sports Lady Blog ilipomtafuta Rage, alikiri kufahamu ujio wa
kocha huyo sambamba na kupanga kukutana naye mwishoni mwa wiki.
Hata hivyo, Rage alishangazwa na madai ya kocha huyo
kutokuwa na taarifa za kutimuliwa kwake kwa madai kwamba analifahamu hilo na
walimpatia barua kabla ya kwenda kwao.
“Nilizungumza naye kabla hajaja na nimepanga kukutana naye
jumapili, hivyo nitakutana naye na kumsikiliza shida yake ni nini juu ya Simba
na baada ya hapo tutaangalia kama tutaitatua au la,”ALISEMA Rage
Aklienda mbali zaidi, Rage alisema kama ni suala la malipo
ya kuvunja mkataba ni jambo la kawaida na haoni ajabu kwa Simba kudaiwa fedha
na mtu ama taasisi yoyote, hivyo ni jambo la kuwa na subira.
“Sisi mbona tunaidai Etoile Du Sahel dola 300,000 za
Emmanuel Okwi lakini kwa vile wametutaka tusubiri basi hatuana budi
kusubiri,”aliongeza Rage
Baada ya kumtema Liewig ambaye alirithi mikoba ya Mserbia
Milovan Cirkovic, Simba iliamua kumpa jukumu la kukinoa kikosi kocha mzawa
Abdallah ‘King’ Kibaden ambaye anasaidiwa na Jamhuri Kihwelo ‘Julio’
Comments
Post a Comment