Press Release
TAMASHA
la Mastaa chipukizi zaidi ya 320 la mwezi Mei litafanyika Jumapili 26, 2013
katika ukumbi wa Starlight Hotel kuanzia saa 4 asubuhi mpaka saa 10 jioni.
Mwenyekiti
wa Shiwata, Caasim Taalib alisema maandalizi ya tamasha hilo yamekamilika na
vikundi vya sanaa vya Kaole, Splendid, Super Shine Taarab, Five Star Modern
Taarab pamoja na wasanii mbalimbali wa Bongo Flava, Maigizo,Ngoma, Dansi na
Sarakasi nao wamethibitisha kushiriki.
Taalib
alisema wasanii wakongwe wa bongo flava walioalikwa ni Stara Thomas, Ommy G na
waigizaji wakongwe wa Kaole na Splendid wataonesha umahiri wao katika fani ya
sanaa Kauli Mbiu ikiwa ni Kilio cha Msanii .
Vikundi
vingine vitakaonesha vipaji vyao ni Kepteni Shaibu, Tanzania Disabled,
Uyoga Boga Village, Ndafu Arts Group, CGC, Magengistar Crew, Dodo Arts Group,
Culture Arts Group, Wachapa Kazi Academy, Soweto Picture, Shiwata Commedy,
Mwavionelachi, Manuari Arts Group, Tandale Morden Taarab na Begeja Wushu,
Wakati
huo huo SHIWATA inawapongeza wote walioshiriki tamasha la
Aprili 27 ambako zaidi ya wasanii 300 walishiriki kuonesha vipaji.
Pia Taalib amelipongeza Shirikisho la Filamu Tanzania
(TAFF) kwa ushirikiano wao mzuri na kuwaomba viongozi wengine wa bendi za
muziki, taarab,vikundi vya sanaa,mapromota,maprodusa na wadau wote kushiriki
katika matamasha haya ili kujenga ushirikiano wa pamoja.
Peter
Mwenda
Ofisa
Habari wa SHIWATA
0715/0752-222677
23/5/2013
Comments
Post a Comment