WAREMBO wanaotarajiwa kushiriki shindano la kumsaka Redd’s
Miss Lindi 2013 wanatarajiwa kuingia kambini jumamosi katika hoteli ya Lindi
Beach Resort kwa ajili ya maandalizi ya shindano hilo litakalofanyika mwezi
ujao.
Mkurugenzi wa kampuni ya Alliance
Entertainment inayoandaa Shindano hilo
Shah Ramadhan, alisema kwamba jumla ya warembo 12 wameshathibitisha kushiriki
shindano hilo.
Alisema warembo hao kutoka wilaya za mkoa huo wanatarajiwa kunolewa
na Miss Pwani 2010, Zainab Mselemu ambapo mwaka huu pia wamejipanga kuhakikisha
kuwa watatoa mwakilishi atakayefanya vema kwenye fainali za Miss Tanzania
baadaye mwaka huu.
“Kama mjuavyo mkoa wa Lindi una historia ya kufanya vema
kwenye fainali za taifa za Miss tanzania kwa miaka tofauti ingawa hatujabahatika
kumtoa Miss tanzania lakini tumeweza kufika hadi tatu bora, kutoa wartembo
wenye vipaji n.k, hivyo naamini na mwaka huu tutafanya maajabu kwani mwaka jana
tu mrembo wetu Irene Veda aliigia 15 bora ya miss Tanzania,”alisema
Shah aliwataja baadhi ya warembo watakaoshiriki shindano
hilo ni pamoja na Asha Abdul, Florida daniel, Mwajuma Juma, Sabra Nanji, Pendo
Chodasi, Leila Abdul, Angel Kisanga, Zainab Shaban, Sophia Maganga na Janet
John.
Aidha, Shah aaliwata wadhamini waliojitokeza mpaka sasa ni
pamoja na Redd's original, Ipinda Trading
co. Ltd,Blue View Hotel, Ndanda springs water,Muhsin General enterprises, Live
trading Center, Mangroove Bar , Big solution, Mtwara cable television Services,
Pride FM Mtwara na Sports Lady Blog.
Comments
Post a Comment