TIGO BLOGGERS PARTY@NEW AFRICA HOTEL


Sports Lady pia niliwakilishaaaaaaaaaaaaaaaa

 Mmoja kati ya wageni waalikwa katika 'Party Mchapalo', iliyowakutanisha wadau wa Mtandano wa Simu za Mkononi Tigo na Wamiliki wa 'Magazeti Mtandao', (Blogers) akichagua kadi wakati ilipokuwa ikichezeshwa droo ya kuwapatia zawadi za Simu za mkononi, Ipad,na Moderm za tigo, mabloger hao, wakati wa hafla hiyo iliyofanyika kwenye Hoteli ya New Africa usiku wa jana(PICHA NA SUFIANI MAFOTO.COM)
 Baadhi ya wamiliki wa mitandao Pendwa, kutoka (kulia) ni mmiliki wa mtandao huu wa Sufianimafoto.com, Dina Ismail Blog, King Kiff Blog na Blogu ya wananchi, wakipozi kwa picha wakati wa hafla hiyo.
 
 Huku ndani wengine walikwishaanza kujisevia yaani 'kujidownlodia' vinywaji na kuapload vinywani mwao kama kawa, kama dawa.
 Kulia ni Meneja wa Mtandao huu Nasma Mafoto, akiwa na shosti wake waliyekutana  katika mchapalo huo.
 Na wanasa kumbukumbu nao hawakuwa nyuma katika kunasa kila tukio lililokuwa likijiri mahala hapo.
 Mwimbaji wa bendi ya Tanzanite, Frola Mkumbo, akiimba kuwaburudisha na kuwapagawisha mabloger, katika hafla hiyo. 
Kina dada nao walichuana kusebeneka na miondoko ya mduara kuwania Ipad na Simu ya mkononi.
Huyu ndiye aliyeibuka kidedea na kuondoka na Ipad...........
 
 Pande hizi wengine kila mmoja alikuwa akijitafuna tu......yaani 'akijiaplodi' vitafunwa.....
 Mr. Mulamula, naye alikuwepo pande hizo akitoa mawili matatu kuwahamasisha mabloger ili kusonga mbele.
 Mzee wa Daladala (kushoto) ndiye alikuwa akisherehesha mchapalo huo pande hizo, (kulia) ni Meneja Mauzo, William....akisubiri kukabidhi zawadi za washindi.
 Mr. William (kulia) akikabidhi zawadi ya Moderm kwa mmoja kati ya washindi wadroo iliyochezeshwa ukumbini hapo.
 Mzee wa Fullshangwe (kushoto) akipokea zawadi ya simu ya mkononi baada ya kujibu swali kwa ufasaha...
 Kajunason (kushoto) naye akipokea zawadi ya Ipad baada ya kuibuka kidedea kwa kuwashinda wenzake katika kusakata sebene na Black Dance...kama Mithun Chakalabot...
 'Snap' ya kumbukumbu.......na wadau wa mitandao.......

Comments