TASWA FC YAWACHAPA FULL MABONDIA FC 2-1, WAKIWA NA MASHALI, MIYEYUSHO, MCHUMIATUMBO

 Kikosi cha Taswa Fc, TIMU ya Taswa Fc jana iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya timu ya Full Mabondia, inayoundwa na mabondia mahiri wa Jijini Dar es Salaam. Timu hizo zilikutana katika mchezo wa kirafiki uliochezwa kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar jana mchana, huku timu ya mabondia ikiwakilishwa na mabondia kama, Thomas Mashali, Mchumiatumbo, Francis Miyeyusho, Majia, Kanda Kabongo, na wengine wengi. Picha zote na www.sufianimafoto.com
 Wadhamini wa timu ya Taswa, Kampuni ya TSN, pia walikuwepo viwanjani hapo wakionyesha kinywaji cha Chilly Willy, kinachotengezwa na kampuni hiyo. Pichani ni baadhi ya warembo wanaotangaza bidhaa za kampuni hiyo, wakiwa katika meza yao.
 Beki wa Taswa Fc, Juma Ramadhan, (nyuma) akimdhibiti mshambuliaji wa Full Mabondia, wakati wa mchezo huo.
 Beki wa Taswa Fc, Muhidin Sufiani 'Sufianimafoto' (kulia) akimfinya mchezaji wa Full Mabondia, wakati wa mchezo huo jana.
 Beki wa Taswa Fc, Elius Kambili, akiambaa na mpira.
 Beki wa Taswa Fc, Salim (kulia) akiondosha moja ya hatari mbele ya Bondia, Mchumiatumbo.
 Kipa wa Full Mabondia, akiwa golini huku akiwa peku peku, wakati wa mtanange huo jana.
 Zahoro Milanzi wa Taswa Fc, (kushoto) akiambaa na mpira wakati wa mtanange huo.
 Wachezaji wa Taswa Fc, wakipasha kabla ya kuanza kwa mtanange huo jana.
Sufianimafoto (katikati) akipozi na Bondia Francis Miyeyusho (kushoto) na 'Chuji' (kulia) kabla ya kuanza kwa mtanange huo jana.
Benchi la Taswa Fc.

Comments