NYOTA wapya
waliosajiliwa katika klabu kongwe za Simba na Yanga wanatarajiwa kuanza
kuonekana kwenye mechi za kirafiki baina ya timu hizo na timu ya Sofapaka ya
Kenya,imefahamika.
Mratibu wa ziara hiyo George Wakuganda alisema jana kwamba
maandalizi ya ujio wa Sofapaka yanaendelea vema ambapo timu hiyo inatarajiwa
kuwasili nchini Juni 10 mwaka huu.
Alisema lengo la
ujio wa timu hiyo ni kuzipa makali Simba na Yanga kabla ya kwenda kushiriki
kwenye michuano ya klabu bingwa Afika Mashariki na Kati maarufu kama Kombe la
Kagame itakayofanyika kuanzia Juni 18 hadi Julai 2 mwaka huu nchini Sudan.
Alisema ikiwa
nchini Sofapaka itakwaana na Simba Juni 12 kabla ya kukipiga na Yanga juni 13
ambapo mechi zote zitafanyika kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Tayari Simba
imeanza mazoezi jana kwenye uwanja wa Kinesi, huku Yanga ambao ni mabingwa wa
Ligi Kuu Bara na watetezi wa michuano ya Kagame wakitarajiwa kuanza kujinoa
Juni 3 mwaka huu.
Comments
Post a Comment