NDOLANGA APONGEZA FIFA KUSIMAMISHA UCHAGUZI TFF, AISHAURI TFF KUTORUDIA MAKOSA


RAIS wa Heshima wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Alhaj Muhidin Ndolanga amelipongeza Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) kwa kubatilisha mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa TFF na kuagiza zoezi kufanyika upya.
Fifa ilifikia uamuzi huo kufuatia kuwepo  baada ya kubaini kasoro iliyotokana na ukosefu wa kutokuwepo vyombo vya kushughulikia ukiukwaji wa maadili.
FIFA ambayo ilituma ujumbe wake katikati ya mwezi uliopita kufanya utafiti kuhusu mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa TFF ambao ulisimamishwa baada ya baadhi ya wagombea kulalamika, imetaka uchaguzi ufanyike kabla ya tarehe 30 Oktoba 2013, lakini ukitanguliwa na mabadiliko ya katiba ambayo yatahusisha uundwaji wa vyombo vya kushughulikia ukiukwaji wa maadkwa utata wa zoezi hilo uliotokana na kuenguliwa kwa baadhi ya wagombea bila ya sababu za msingi, huku pia mchakato huo ukiendeshwa kwa katiba batili.
Akizungumza kwenye kipindi cha Spoti leo kinachorushwa na Redio One juzi, Ndolanga alisema hadhani TFF kama itavurunda tena zoezi hilo kama ilivyokuwa awali.
Ndolanga ambaye alikuwa ni mmoja ya wadau waliohojiwa na Fifa juu ya utata wa uchaguzi huo alisema kwamba, anaamini TFF itajipanga vizuri katika hilo ili haki iweze kutendeka kwa kila mmoja.
“Sidhani kama hivi sasa tutaendeleza matatizo ya awali, Katiba ilivunjwa na kubadilishwa kwa waraka hivyo naamini itarekebishwa kwa mujibu wa taratibu na kisha tuendelee na taratibu nyingine.
Aidha, Ndolanga alitoa rai kwa wajumbe wa mkutano mkuu kuwa makini katika zoezi la kubadilishwa kwa katiba ya TFF  kwa kuhakikisha wanaingiza vitu ambavyo vitaleta faida kwa Taifa zima la Tanzania.

Comments