KOCHA MKUU TP MAZEMBE ABWAGA MANYANGA


KOCHA mkuu wa klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidem,okrasia ya Congo (DRC) Lamine Ndiaye ametangaza kujiuuzulu wadhifa wake huo.
Taarifa ya klabu hiyo iliyotolewa jana imeeleza kwamba kocha huyo ameamua kuachia ngazi baada ya klabu hiyo kutupwa nje kwenye michuano ya CAF.
Rais wa klabu hiyuo Moses Katumbi,alitangaza uamuzi wa kocha huyo kujitoa kuifundisha klabu hiyo na kusema kuwa hawana budi kukubaliana na uamuzi huo.
Hata hivyo, Rais huyo amezuiia kuondoka kwa kocha huyo na kumpatia kazi nyingine ndani ya klabu hiyo.

Comments