Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linaitakia kila
la kheri timu ya Azam katika mechi yake ya michuano ya Kombe la Shirikisho
barani Afrika itakayochezwa nchini Morocco leo.
Mechi hiyo ya marudiano ya raundi ya pili ya michuano hiyo
itachezwa jijini Rabat kuanzia saa 11 jioni kwa saa za Morocco. Timu hizo
zilitoka suluhu katika mechi ya kwanza iliyochezwa jijini Dar es Salaam wiki
mbili zilizopita.
Azam iko nchini Morocco kwa karibu wiki nzima sasa
ikijiandaa kwa mechi hiyo chini ya Kocha wake Stewart John Hall. Msafara wa
Azam nchini humo unaongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, Eliud
Mvella.
Comments
Post a Comment