Nahodha wa timu ya
Simba, Juma Kaseja ameweka sharti la kupatiwa kitita cha dola 40,000 (sh mil
64) ili asaini mkataba mpya.
Kaseja
ambaye pia ni kipa namba moja wa timu hiyo aliyeitumia zaidi ya miaka 10,
mkatabata wake unamalizika mwezi huu.
Habari
kutoka ndani ya klabu ya Simba zinasema kwamba, nyota huyo ametaka kiasi hicho
cha fedha ili aweze kuongeza mkataba mwingine wa kuitumikia klabu lakini
haitawezekana kwani ni dau kubwa.
Kiongozi
mmoja wa Simba ambaye hakupenda kutajwa jina lake, alidokeza jana, ingawa bado
wanamhitaji kipa huyo, kiasi anachotaka ni kikubwa.
“Kweli
bado tunamuhitaji Kaseja, lakini kwa hali iliyopo hatuna kiasi hicho cha fedha.
Ngoja tusubiri amalize majukumu yake ya kuitumikia timu ya Taifa halafu tutakaa
naye na kuzungumza,”alisema.
Hata
hivyo, taarifa kutoka kwa mtu wa karibu wa Kaseja zinaeleza, hata kama uongozi
utaafikiana naye kuhusiana na mkataba wake, kuna mambo anataka yawekwe sawa.
Moja
ya mastarti hayo ni kuhakikishiwa kwa nafasi yake ndani ya klabu hiyo, pamoja
na uongozi kutoingilia benchi la ufundi.
“Unajua
Kaseja ameona kuna mambo kadhaa ya kuzungumza na uongozi kwanza ili yaweze
kumlinda katika mkataba wake,”alisema
Kaseja
ambaye alikuwa tishio katika miaka ya nyuma kiasi cha kupachikwa jina la
‘Tanzania One’ katika siku za hivi karibuni kiwango chake kimeonekana kushuka.
Baada ya kuona hali hiyo, uongozi wa Simba katika
dirisha dogo la usajili ilimsajili kipa
Comments
Post a Comment