Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limemteua
Leslie Liunda wa Tanzania kuwa mtathmini wa waamuzi (referee assessor) katika
mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia.
Mechi hiyo ya Kundi B, Kanda ya Afrika kati ya Cape Verde na
Equatorial Guinea itafanyika Juni 8 mwaka huu saa 10.30 jioni kwenye Uwanja wa
Verzea mjini Praia.
Waamuzi wa mechi hiyo ambao watatoka Angola ni Martins De
Carvalho Helder, Dos Santos Jerson Emiliano, Da Silva Lemos Julio na
Muachihuissa Caxala Antonio. Kamishna wa mechi hiyo atakuwa Diarra Massa Momoye
wa Mauritania.
Comments
Post a Comment