WASANII chipukizi 300 kutoka vikundi 15
jijini Dar es Salaam wamejitokeza kushiriki maonesho ya kukuza vipaji
yaliyoandaliwa na Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA) Jumamosi ya Aprili 27
katika ukumbi wa hoteli ya StarLight ,Mnazi Mmoja Dar es
Salaam.
Vikundi ambavyo
vimethibitisha kushiriki pamoja na Kaole Sanaa Group,Splendid,Uyoga Boga na
vingine katika fani ya Bongo Flava,Taarab,Maigizo,Ngoma,Mazingaombwe,Sanaa za
Ufundi,Kung Fu,Sarakasi,Kusheki,Kwaya,na Ngonjera.
Maonesho kama haya
yatafanyika kila mwezi na kiingilio ni bure na vikundi vingine ni Super Shine
Morden Taarab,Zijiu,Edeneza Brass Band,Asili Africa,Mege Arts,Kintu,Army
Kwanza,Wachapakazi,Tanhope,Tanz Arts,Mshikamano,Big House,Lutenga
Boys,Kilimasta,Manuary.
Madhumuni makubwa ya tamasha hilo ni kuibua
vipaji vya wasanii chipukizi ili kazi zao ziweze kupata soko hivyo mapromota,
Majd,Maproducer wa filamu wasikoke kufika katika maonesho hayo ili kuona mastaa
chipukizi ambao ambavyo vipaji vyao bado havijaonekana.
Vijana wa sanaa
mbalimbali wanatakiwa kufika katika ofisi za SHIWATA zilizopo Bungoni Ilala ili
kujisajili kwa ajili ya maonesho mengine yanayofuata .
Tanzania kuna
wasanii wengi wenye vipaji lakini kazi zao hazisikiki wala kuonekana kwenye
vyombo vya habari hivyo hiyo ni fursa kutumia maonesho hayo kama soko la kazi
zao katika jiji la Dar es Salaam.
Wasanii mbalimbali
ambao vipaji vyao vitakubalika sokoni watanufaika kupata ajira ya kuuza kazi zao
pamoja na kushiriki katika matamasha mbalimbali ndani na nje ya
nchi.
Peter
Mwenda
Ofisa Habari wa
SHIWATA
0715/0752
222677
Comments
Post a Comment