SHIRIKISHO la Soka Tanzania
(TFF), limetoa wito kwa wachezaji wa Tanzania wanaoziwakilisha klabu zao kwenye
michuano ya kimataifa, kuonesha nidhamu nzuri uwanjani ili kuepuka adhabu ya
kadi nyekundu.
Hatua hiyo inatokana na Shirikisho
la Soka Afrika (CAF), kutoa kanuni mpya, ambapo mchezaji atakayepata adhabu ya
kadi nyekundu ataitumikia pia katika timu yake ya taifa.
Katibu Mkuu wa TFF, Angetile
Osiah, alisema jijini Dar es Salaam jana kwamba kwa hali hiyo, wachezaji hawana
budi kuwa makini wawapo uwanjani, kwani adhabu hiyo itakuwa ni hasara kwa taifa
pia.
Alisema ni muhimu kwa
wachezaji wa timu husika kucheza kwa kufuata sheria 17 za soka ili kuepukana na
adhabu hiyo itakayomfanya ashindwe kuitumikia pia timu ya Taifa.
Comments
Post a Comment