KOCHA Tom Saintfiet aliyeipa
Yanga ubingwa wa Kombe la Kagame Julai 28, mwaka jana kwa kuifunga Azam mabao
2-0, ameomba kazi ya kuinoa timu ya taifa ya Uganda kuziba nafasi ya Bobby
Williamson aliyetimuliwa baada ya kuinoa timu hiyo kwa miaka mitano.
Williamson raia wa Scotland ametimuliwa kazi kutokana na timu hiyo
kutopata matokeo mazuri katika kampeni ya kucheza fainali za Kombe la Dunia
hapo mwakani nchini Brazil .
Saintfiet, aliyewahi kuinoa
timu ya taifa ya Namibia kwa
miaka miwili na nusu kabla ya kuzinoa pia Ethiopia
na Yemen ,
anaamini anaweza kuipatia mafanikio timu hiyo ya ukanda wa Afrika Mashariki.
“Nimekuwa nikiifutilia soka
ya Uganda
kwa miaka kadhaa. Ni kati ya timu zinazocheza soka ya kuvutia katika ukanda
huku wachezaji wake wakiwa na vipaji vya kutosha,” alisema na kuongeza:
“Nilipokuwa nainoa Ethiopia , niliwaona wakicheza mechi za Cecafa na
nilipokuwa nainoa Yanga ya Tanzania ,
nilikuwa na wachezaji wa Uganda
katika timu, ni wachezaji wazuri sana
ambao walikuwa msaada kwa timu kutwaa ubingwa Kagame mwaka jana,” alisema Sainfiet.
Saintfiet (40), alisema kwa
mazingira hayo, kitendo cha Uganda
kutocheza michuano ya mikubwa kama Kombe la
Mataifa Afrika, ni kukosa bahati tu.
“Lakini sasa ni muda wa
kusonga mbele zaidi,” alisema na kuongeza: “Wanaweza, nataka kuwasaidia. Uganda ni pekee yenye pointi tatu kwenye kampeni
za kucheza fainali za kombe la Dunia nyuma ya vinara, kama itasghinda mechi
mbili za nyumbani dhidi ya Liberia
na Angola
hapo Juni, itakuwa kwenye nafasi nzuri,” alisema.
“Mwakilishi wangu amezungumza
na rais wa Fufa-Shirikisho la soka Uganda
(Mulindwa) ameonekana ni kiongoni mwenye kiu ya mafanikio ya soka kwa nchi
yake, nasubiri kuitwa, naamini nikifanikiwa tutashirikiana kujenga timu imara
zaidi kuelekea Kombe la Dunia na Fainali zijazo za Mataifa Afrika za Morocco ,”
Saintfiet mwenye cheti cha
daraja la juu katika ufundishaji kinachotambuliwa na Shirikiisho la soka Ulaya
(Uefa),
alianza kufungisha mchezo huo
miaka 17 iliyopita.
Amewahi kuwa Mkurugenzi wa
Ufundi wa Shirikisho la soka Nigeria
kabla ya kutema kibarua hicho kutokana na
malipo yake kuzua mzozo.
Comments
Post a Comment