AZAM FC jana walizidi kuichimbia kaburi la
kushuka daraja, African Lyon baada ya kuilaza mabao 3-1 katika mchezo wa Ligi
Kuu ya Vodacom, uliopigwa dimba la Chamazi Complex, Mbagala jijini Dar es Salaam,
Mcha Khamis Mcha ‘Viali’, Kipre
Tchetche ambaye alifunga mawili, huku lile la Lyon lilifungwa na Adam Kigwande
Kwa
ushindi huo, Azam imezidi kuwafukuzia vinara wa ligi hiyo Yanga wenye pointi
49, baada ya kufikisha pointi 46, lakini ipo mbele mchezo mmoja.
Kwa
upande wa Lyon, imezidi kuchungulia daraja la kwanza, ikibakia na pointi zake
19 baada ya kushuka dimbani mara 23 ikiwa nafasi ya pili kutoka mkiani.
Mara
baada ya filimbi ya mwisho ya mwamuzi, Godfrey Tumaini, Kocha wa Lyon, Charles
Otieno, alijitosa uwanjani kumvaa akidai kuipendelea Azam, lakini Polisi
walimdhibiti na kumtoa nje ya uwanja.
Comments
Post a Comment