YANGA YABANWA NA MAAFANDE WA MORO


VINARA wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Yanga SC leo wamepunguzwa kasi baada ya kulazimishwa sare tasa na  wenyeji Polisi, mchezo uliopigwa kwenye dimba la Jamhuri Mjini Morogoro. 
Matokeo ya leo yameifanya Yanga kutibua rekodi yake  ya kushinda mechi zake zote tangu kuanza kwa mzunguko wa pili wa ligi hiyo. 
Katika mchezo huo, timu hizo ziliunza mchezo kwa kusomanana  ambapo  Yanga ilipata kona dakika ya 13, 26, 31, 43 na 45 huku Polisi Moro ilipata kona katika dakika ya 10, 27,37 na 41.Kona zote hazikuzaa matunda.
Katika dakika ya 24 amanusra kiungo wa Mokili Rambo atiukise nyavu za Yanga kabla ya beki Mbuyu Twite kuokoa mchomo huo ukiwa  unaelekea nyavuni. 
Aidha, Kipa wa Polisi, Kondo Salum alifanya kazi ya ziada dakika ya 26 kupangua mpira wa kichwa wa beki wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ kufuatia kona maridadi ya David Luhende. 
Mshambuliaji wa Yanga, Said Bahanuzi ‘Spider Man’ aliikosa  bao la wazi, baada ya kuchelewa kuiwahi krosi nzuri ya Simon Msuva na mpira ukapitiliza hadi mikononi mwa kipa wa Polisi.Na hivyo kumaliza kipindi cha kwanza kwa 0-0. 
Kipindi cha pili kilianza kwa kila timu kusaka bao kwa  udi na uvumba, huku Polisi wakiutawala zaidi mchezo lakini walishindwa kuzitendea haki nafasi za wazi walizozipata . 
Katika dakika  ya 51, Mbuyu Twite alipewa kadi ya njano baada ya kupuuzia maamuzi ya mwamuzi wa mchezo huo Dominic Nyamisana kutoka Dodoma. 
Yanga ilimtoa Nizar Khalfan, Said Bahanuzi na kumuingiza Stephano Mwasika na Didier Kavumbagu, huku polisi wakimtoa Mokili Rambo na kumuingiza Keneth Masumbuko. 
Kwa matokeo hayo Yanga imefikisha pointi 49, ikifuatiwa na Azam Fc yenye pointi 43 na Kagera Sugar ikiwa ya tatu kwa pointi 37.

Yanga SC ; Ally Mustafa ‘Barthez’, Mbuyu Twite, David Luhende, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Athumani Iddi ‘Chuji’, Simon Msuva, Frank Domayo, Said Bahanuzi/Didier Kavumbangu , Hamisi Kiiza na Nizar Khalfan/Stefano Mwasyika dk46.

Polisi Moro; Kondo Salum, Rodgres Freddy,  Castro Ngwangila, Chacha Marwa, Salmin Kiss, Nahoda Bakari, Bantu Admin, Muzamil Yassin, Mokili Rambos/Kenneth Masumbuko dk 75, Machaku Salum na Nicholas Kabipe.

Comments