Taifa Stars imeanza kambi jana jioni (Machi 16 mwaka huu)
ambapo wachezaji 14 kati ya 23 walioitwa wameripoti na kufanya mazoezi leo
asubuhi chini ya Kocha Kim Poulsen.
Wachezaji walioripoti ni nahodha Juma Kaseja kutoka Simba na
msaidizi wake Aggrey Morris wa Azam, Erasto Nyoni (Azam), Kelvin Yondani
(Yanga), Nadir Haroub (Yanga), Nassoro Masoud Cholo (Simba), Shomari Kapombe
(Simba) na Salum Abubakar (Azam).
Wengine ni Athuman Idd (Yanga), Amri Kiemba (Simba), Frank
Domayo (Yanga), Mwinyi Kazimoto (Simba), Mrisho Ngasa (Simba) na Simon Msuva
(Yanga).
Wachezaji Hussein Shariff, Issa Rashid na Shabani Nditi
ambao timu yao ya Mtibwa Sugar jana ilicheza mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL)
mjini Turiani wataripoti kambini leo jioni.
Kikosi hicho kitakamilika Jumanne asubuhi baada ya wachezaji
walio katika kikosi cha Azam nchini Liberia kwenye mechi ya Kombe la Shirikisho
kurejea nchini. Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wanaochezea TP Mazembe ya
Jamhuri ya Kidemorasi ya Congo (DRC) wanatarajiwa kutua nchini kesho usiku.
Comments
Post a Comment