STARS IPO TAYARI KUIVAA MOROCCO, MASHABIKI WATAKAOINGIA NDANI YA UWANJA KUKIONA


WAKATI kikosi cha timu ya soka ya Taifa ‘Taifa Stars’ kikiwa tayari kuivaa Morocco keshokutwa, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limepiga marufu mashabiki kuingia ndani ya uzio wa uwanja.
Stars na Morocco zitakwaana kesho katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam katika mechi ya y Mchujo ya kuwania tiketi ya kucheza fainali za kombe la dunia zitakazopigwa mwakani nchini Brazil.
Ofisa habari wa TFF Boniface Wambura,  alisema kwamba wachezaji wote 23 walioitwa kwenye kikosi cha Stars wapo katika hali nzuri na wanaendelea na mazoezi yao chini kocha mkuu Kim Poulsen.
Alisema kwa kiasi kikubwa kambi ya Stars iliyopo kwenye Hoteli ya Tansoma katikati ya jiji la Dar es Salaam inaendelea vizuri huku wachezaji wakiwa na ari kubwa ya kutaka kushinda mchezo huo utakaopigwa kuanzia saa tisa alasiri.
Wachezaji wanaounda kikosi cha Stars ni pamoja na  makipa Juma Kaseja ambaye pia ndiye nahodha wa Stars, Aishi Manula( Azam ), Hussein Shariff (Mtibwa Sugar) na Mwadini Ally (Azam). Huku  Mabeki ni Aggrey Morris (Azam), Erasto Nyoni (Azam), Issa Rashid (Mtibwa Sugar), Kelvin Yondani (Yanga), Nadir Haroub (Yanga), Nassoro Masoud Cholo (Simba) na Shomari Kapombe (Simba).
Kwa upande wa Viungo ni Salum Abubakar (Azam), Athuman Idd (Yanga), Amri Kiemba (Simba), Khamis Mcha (Azam), Frank Domayo (Yanga), Mwinyi Kazimoto (Simba) na Shabani Nditi (Mtibwa Sugar). Wakati Washambuliaji ni John Bocco (Azam), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Mrisho Ngasa (Simba), Simon Msuva (Yanga), na Thomas Ulimwengu wa TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC).
Kuhusiana na Mashabiki watakaokiuka onyo la TFF kwa kuingia kwenye uzio wa Uwanja wa Taifa, Wambura alisema mashabiki watakaokiuka watachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kufungiwa kuingia katika uwanja huo.
Aidha, Wambura alisema kikosi kingine cha  Morocco kilitarajiwa kuwasili jana tayari kwa mchezo huo, ambapo kundi la kwanza lililowasili juzi na kufikia kwenye hoteli ya  Kilimanjaro Hyatt Regency ambapo leo itafanya mazoezi yake ya mwisho kwenye Uwanja wa Taifa kuanzia saa 9 alasiri.
Kikosi cha Morocco kinachonolewa na kocha  Kocha Rachid Taoussi  kinaunnwa na  Nadir Lamyaghri, Anas Zniti, Yassine Bounou, Younnes Bellakhadar, Abdellatif Noussair, Abderrahim Achchakir, Zoheir Feddal, Younnes Hammal, Zakarya Bergdich na Abdeljalil Jbira.
Pia wamo Issam El Adou, Kamel Chafni, Salaheddine Saidi, Mohamed Ali Bamaamar, Abdelaziz Barrada, Salaheddine Aqqal, Abdessamad El Moubarky, Nordin Amrabat, Chahir Belghazouani, Abdelilah Hafidi, Youssef Kaddioui, Brahim El Bahri, Hamza Abourazzouk na Youssef El Arabi.

Comments