Washiriki wa warsha ya kujadili na kuboresha mkakati wa
Mawasiliano wa Wizara ya Fedha, kutoka vyombo vya Habari mbalimbali nchini
wakijadiliana leo katika ukumbi wa Kilimanjaro Park Hotel, Kibaha mkoani Pwani.
Kulia ni Othman Michuzi wa Mtaa kwa Mtaa Blog, akiwa na Dina Ismail wa Sports Lady Blog kushoto wakisikiliza kwa makini mjadala huo.
Baadhi ya wamiliki wa mitandao ya kijamii wakiwa katika
picha ya pamoja.(Picha kwa Hisani ya Mtaa kwa Mtaa Blog)
Kushoto ni Thabit Matotola kutoka kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Fedha na kulia Anthony Siame kutoka kampuni ya New Habari
Baadhi ya maofisa toka wizara mbalimbali nchini wakijadiliana katika warsha hiyo iliyofanyika kwenye hoteli ya Kilimanjaro Park iliyopo Misugusugu, Kibaha mkoani Pwani.
Kulia ni Othman Michuzi wa Mtaa kwa Mtaa Blog, akiwa na Dina Ismail wa Sports Lady Blog kushoto wakisikiliza kwa makini mjadala huo.
Kushoto ni Thabit Matotola kutoka kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Fedha na kulia Anthony Siame kutoka kampuni ya New Habari
Kulia ni Mahmoud Zubeiry wa Bin Zubeiry Blog akiwa na Henry
Mdimu wa gazeti la Mwananchi na Ahmed Michuzi wa Jiachie Blog
Na Sports Lady, Kibaha
IMEBAINIKA kwamba bado kuna baadhi
ya umuhimu wa kurejeshwa kwa vituo vya kijamii (Community Centres) ili kuwezesha wananchi wote nchini kuweza
kupata habari.
Hayo yalibainika mwishoni mwa
wiki iliyopita wakati wa warsha ya siku moja kuhusu njia mbadala ya kufikisha
taarifa za kimaendeleo kwa wananchi iliyoandaliwa na Wizara ya Fedha na
kushirikisha wamiliki wa mitandao ya
kijamii (Blogs), maofisa habari kutoka idara mbalimbali na wadau wengine.
Wakichangia mada, wadau hao
walidai kuwa licha ya kuwepo kwa utandawazi lakini kuna baadhi ya jamii na hasa
za vijijini bado hazipati taarifa za matukio mbalimbali yanaoondelea katika
ulimwengu huu.
Walisema hiyo inatokana na
njia zinazotumika kutangaza hizo taarifa kutowafikia wengi kama inavyodhaniwa
na hivyo bado kuna haja ya kurejeshwa vituo vya kupashana habari kama ilivyokuwa zamani.
“Sidhani huko vijijini kama
kila mtu anauwezo wa kuliki simu ya mkononi au kuwa na uwezo wa kujiunga na
mitandao ya kijamii, hivyo basi ni ngumu jamii hiyo kupokea taarifa mbalimbali
za kimaendeleo hususani kama hizi za kibenki,”
“Zamani nakumbuka kulikuwa na
siku na sehemu maalum watu wanakutana na kuangalia sinema mbalimbali kama
ambazo zilikuwa ni maalum kwa kufikisha ujumbe fulani kwa jamii kama ukimwi n.k lakini hayo siku hizi hakuna, hivyo
nadhani serikali ama mashirika yangetilia mkazo kurudisha mkakati huo,”waliongeza
wadau hao
Wakienda mbali zaidi, wadau
hao walisema kikwazo kingine ni lugha kwani kuna baadhi ya kampeni zinaendeshwa
kwa lugha ya kiingereza kitua ambacho si wote wanaoifahamu kwa ufasaha lugha
hiyo, pia kuna maeneo hata lugha ya Kiswahili hawaielewi zaidi ya lugha
ya eneo husika hivyo ingekuwa bora hata kampeni hizo zikafikishwa maeneo hayo
zikiwa katika lugha ya eneo husika.
Awali, akifungua warsha hiyo iliyofanyika kwenye Hoteli ya Kilimajaro Park iliyopo Misugusugu, Kibaha mkoani
Pwani, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha Wizara ya Fedha, Ingiahedi Mduma, alisema ni haki ya
kila mwananchi kujua taarifa za kimaendeleo za nchi hivyo wameamua kukaa chini na kutafuta njia mbadala
ya kuiona ni jinsi gani taarifa hizo zitawafikia wananchi.
Comments
Post a Comment