Simba leo imelazimka kugawana
pointi na wenyeji Toto African ya Mwanza baada ya sare ya mabao 2-2, katika
mchezo uliopigwa Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza.
Sare hiyo imeifanya Simba
kushuka nafasi moja chini kutoka ya tatu hadi ya
nne kwani matokeo hayo yameifanya kufikisha pointi 34, baada ya jana Kagera
Sugar kuwatandika mabao 2-1 ndugu zao, Mtibwa Sugar.
Katika mchezo huo ambao
ulitawaliwa na rafu za hapa na pale, Simba ambayo imeonekana kusuasua katika
mechi zake za duru hilo
la lala salama, ilionesha kiwango cha chini.
Toto ndio walianza kuandika
kalamu ya mabao katika dakika ya 24 kupitia kwa Musa Said aliyepiga shuti kali nje ya 18 na kutinga moja kwa moja
nyavuni.Dakika tatu baadaye Said Mkopi aliisawazishia Simba baada ya kuitendea haki krosi ya Haruna Chanongo.Timu hizo
zilikwenda mapumziko kwa sare ya bao 1-1.
Katika mchezo huo wachezaji
wa Simba Jonas Mkude na Adam Miraji walilimwa kadi ya njano kwa kuwachezea
vibaya wac hezaji wa Toito.
Dakikaya 36 Toto walishindwa
kutumia nafasi nyingine waliyoipata kupitia kwa Evarist Maganga aliyeunganisha
kwa kichwa mpira wa kona uliopigwa na
Emmanuel Swita na kutoka nje.
Dakika ya 40 Simba ilimtoa
Jonas Mkude na kumuingiza Ramadhan Salum
Mshambuliaji wa Simba Mrisho
Ngasa aliyeingia dakika ya 55 akichukua nafasi ya Mkopi aliwainua mashabini wa
timu hiyo katika dakika yya 62 mara baada ya kufumua shuti kali nje ya 18.
Dakika ya 68 shabiki wa Simba alikubali kichapo kutoka kwa shabiki
wa Yanga mara baada ya kuzunguka uwanja na pikipiki akiwa na bendera na ndipo
shabiki wea Yanga aliposhuka jukwaani na kuing’oa bendera na shabiki huyo kushuka kwenye pikipiki na
kwenda jukwaani ambapon alikumbana na kichapo hicho.
Selemani Kibuta
aliisawazishia Toto dakika ya 72 baada ya mabeki wa Simba SC
kujichanganya na kumpa mwanya mshambuliaji huyo wa Toto kufunga, aliyeingia
kipindi cha pili kusawazisha.
Simba: Juma Kaseja, Nasoro Masoud ‘Cholo’, Miraj Adam,
Shomari Kapombe, Hassan Khatib, Jonas Mkude, Amri Kiemba, Abdallah Seseme,
Rashid Mkopi, Ramadhani Singano ‘Messi’, Haruna Chanongo.
Toto African: Erick
Ngwengwe, Erick Muliko, Robert Magadula, Evarist Maganga, Hamis Msafiri, Musa
Msafiri, Emmanuel Swita, Henry Khalifa, James Magafu, Mohamed Jingo, Erick
Kyaruzi.
Comments
Post a Comment