TIMU ya soka ya Ruvu Shooting
imesema ipo tayari kwa mchezo wake wa ligi kuu bara dhidi ya vinara wa ligi
hiyo, Yanga utakaopigwa kesho kwenye dimba la Taifa jijini dar es salaam .
Akizungumza jijini Dar es
Salaam jana, ofisa habari wa Ruvu Shooting, Masau Bwire alisema kwamba timu
hiyo inayonolewa na makocha Boniface Mkwasa akisaidiwa na seleman Mtungwe
imedhamiria kushinda mchezo huo ili kujiweka katika mazingira ya kuwania
ubingwa.
Alisema Ruvu Shooting
haiidharau yanga inayoshikilia usukani wa ligi hiyo lakini uwezo wa kusakata
kabumbu walionao wachezaji wake unawapa kujiamini na uhakika wa kushinda mchezo
huo.
“Tumejipanga vema ili kuweza
kushinda mchezo huo, tunafahamu kutakuwa na ushindani wa hali ya juu kwani
Yanga ni timu nzuri pia lakini dhamira ya kuiondoka na pointi tatu ipo
palepale,”alisema Bwire
Bwire aliongeza kuwa wanataka
kuwadhihirishia Watanzania kwamba soka la Tanzania
si la Yanga na Simba, bali zipo timu zenye uwezo wa kucheza zaidi yao hususani Ruvu Shooting
pale itakapoibukiza mabao ya kutosha Yanga katika mchezo wa kesho.
Aliongeza kuwa pamoja na
tambo za ‘Wazee hao wa Uturuki’ kwa kutofungwa tangu waliporejea kutoka Uturuki
kuweka kambi ya maandalizi na kudai hawatofungwa na timu yoyoyote, wanataka
kuanza kuuvunja mwiko wao huo na matokeo
yao kuishia
kuitwa ‘Wapiga debe wa manzese’.
Aidha, Bwire aliomba mwamuzi
wa mchezo huo kuchezesha kwa kufuata sheria 17 za soka na mshindi apatikane kwa uwezo wa uwanjani na si kubebwa.
“Nawaomba mashabiki
kujitokeza jkwa wingi uwanjani hususani mashabiki wa Simba watakaofarijika na
matokeo hayo kuja kushuhudia maarifa ya
sisimizi kumuua tembo, “alisema
Katika hatua nyingine, Bwire
alisema wameandika barua kwa Shirikisho la Soka tanzania (TFF) kuomba kuvaa
vitambaa vyeusi kwenye mkono wa kushoto pamoja na kusimama dakika moja kabla ya
mchezo kwa ajili ya maombolezio ya kifo cha mlezi wao Luteni Simon Thomas.
Bwire alisema Thomas
aliseyerkuwa mlezi wa kikosi cha 832 Ruvu JKT alifariki juzi akiwa njiani
kwenda hospitali na leo mwili wake utasafirishwa kwenda kwao Musoma kwa
mazishi.
Comments
Post a Comment