Mwenyekiti wa Simba Al Hajj Ismail Aden RAge akizungumza na wanachama pamoja na mashabiki wa Simba hii leo mara baada ya kurejea kutoka nchini India alipokwenda kwa ajili ya matibabu.
Baadhi ya mashabiki wakimsikiliza Rage
Baadhi ya mashabiki wakimsikiliza Rage
Baadhi ya mashabiki wakimsikiliza Rage
Baadhi ya mashabiki wakimsikiliza Rage
Baadhi ya mashabiki wakimsikiliza Rage
Baadhi ya mashabiki wakimsikiliza Rage
Baadhi ya mashabiki wakimsikiliza Rage
Na Dina Ismail
MWENYEKITI wa klabu ya Simba Alhaj Ismail Aden Rage amesema
kuwa chokochoko zinazoendelea ndani ya klabu hiyo inatokana na tamaa ya dola
300,000 za mauzo ya aliyekuwa mshambuliaji wa timu hiyo Emmanuel Okwi aliyeuzwa
katika klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia.
Aidha, Rage amesisitiza kuwa hakuna kitu kinachoitwa
mapinduzi ndani ya klabu hiyo na kwamba anawasubiri kwa hamu leo makao makuu ya
klabu hiyo wale waliotangaza kumpindua.
Akizuingumza na mashabiki na wanachama wa klabu hiyo jioni ya leo makao makuu ya klabu mitaa ya Msimbazi na Twiga mara baada ya kurejea kutoka
nchini India alipokwenda kwa matibabu, Rage alisema wanaoleta matatizo ndani ya
klabu hiyo ni wale wenye utu wa kujil;imbikizia mali.
Alisema chini ya uongozi wake Simba imefanya mambo ya uwazi
na ukweli ikiwamo hilo suala la kuuza wachezaji ambapo fedha zimeonekana
tofauti na waliomtangulia kwani walipowuza wachezaji ferdha ziliyeyuka.
“Tumemuuza Samata (Mbwana) , tumemuuza Ochan (Patrick) fedha
zimeoonekana lakini je wao walipowauza kina Henry Joseph, Haruna Moshi (Boban),
Danny Mrwanda, na wengineo klabu ilipata sh ngapi?
Rage aliongeza kuwa chini ya uongozi wake wamewezesha
kupatikana kwa fedha kupitia kodi ya pango ya jengo hilo ambapo awali ilikuwa
sh 200,000 lakini sasa imepanda hadi milioni 2 na hiyo pia ni sababu inayowapa
tamaa watu hao weasioitakia mema.
Akienda mbali zaidi Rage alisema kama kundi hilo lililofanya
mapinduzi lingekuwa halali hata watu wqaliowateua kuongoza kwa muda Zacharia
Hans Poppe na Rahma Al Kharoos ‘Malikia wa Nyuki’ wasingewakatalia kukalia hayo
madaraka yao ya muda.
Rage alisema kwa sasa
uongozi umedhamirtia kuiletea mafanikio timu hiyo kongwe kama huku akisema ni
aibu kwa hali iliyonayo pamoja na ukongwe huo ukilinganishga na Azam hayo jana
kwenye makao makuu ya klabu hiyo mara baada ya kuwasili kutoka nchini India
alipokwenda kwa ajili ya matibabu.
“Angalia Azam ina miaka 10 tu katika ulimwengu wa soka ina
mafanikio makubwa, lakini Siumba ina miaka 70 hakuna cha maana tyulichofanya
lazima tuone aibu,”aliongeza
Hivi karibuni zaidi ya mashabiki 700 wa timu hiyo waliitisha
mkutano mkuu wa dharula na kuadhimia kumng’oa Rage na wenzake kwa madai ya
kushindwa kuiongoza klabu hiyo kiasi cha kufanya timu ya Simba kufanya vibaya
kwenye mechi zake za Ligi Kuu ya Vodacom kabla ya kutolewa katika hatua ya pili
ya kombe la Shirikisho barani Afrika.
Comments
Post a Comment