PASCAL 'KIMONDO' NDOMBA:BONDIA WA TANZANIA ALIYEPATA ULAJI KWA OBAMA

Na Dina Ismail
PAMOJA na kutojulikana sana hapa nchini lakini ubora alionao bondia Pascal Ndomba maarufu kama ‘Kimondo’ amefanikiwa kupata ulaji nchini Marekani.
Kimondo bondia mwenye makazi yake nchini Martekani amelamba dili ya kufanya kazi kwa miaka minne katika kampuni ya Nelson Promotion ya Miami, nchini Marekani.
Katika mahojiano na mwandishi wa makala haya, Kimondo pamoja na kumshuru mungu anasema atafanya jitihada zote kuhakikisha anaipeperesha vema bendera ya Tanzania.
Anasema kwa muda mrefu amekuwa na ndoto za kuipeperusha bendera ya Tanzania kupitia mchezo huo, hivyo kwa nafasi aliyoipata hatofanya makosa.
Kimondo anasema alipata dili hilo baada ya mmliki wa kampuni hiyo kumshuhudia akizipiga na Mrusi Issa Akberbaew lililofanyika Urusi mwaka 2011 na kudundwa.
“Mpinzani wangu alinizidi uzito ndiyo maana aliweza kushinda, hata hivyo Nelson Promotion waliridhishwa na kiwango change na kuondelea kunifuatilia zaidi katika mapambono tofauti’, anasema.
Bondia huyo anasema kuwa  alikipiga na Agron De Zilla wa Uswisi na kuchapwa katika pambano lililofanyika Uswisi na bada ya hapo wamiliki wa Nelson Promotion walimfuata na kutaka kufanya naye kazi.
Anaongeza kuwa baada ya kukubaliana na kampuni hiyo alitakiwa kujiunga na kituo chao maalum cha mazoezi kilichopo Marekani ambapo huko alikutana na mabondia kutoka nchi tofauiti kama Mexico, Cuba, Marekani na nyinginezo.
Akiwa huko pamoja na mazoezi pia alikuwa akipatia lishe maalum ambayo itamuzesha kupungua uzito ili kufikia unaotakiwa na aliweza kupungua kutoka kilo 81 hadi kufikia kilo 72.
“Yaani kule ni mazoezi tu na pia kuna wataalamu wanaosimamia lishe ili kumfanya bondia apate uzito unaostahili,”anaongeza.
Anasema baada ya uongozi kuridhishwa na kiwango alichofikia katika kituo hicho ikiwemo kupungua uzito, alifanyiwa vipimo vya afya na baada ya kuonekana yupo fit ndipo walipomsainisha makataba wa kufanya nae kazi.
Kimondo anasema baada ya kupata dili hilo anatarajiwa kupanda ulingoni kwa mara ya kwanza Aprili 20 mwaka huu katika ulingo wa MGM huko Florida, Marekani kukwaana na bondia wa huko katika pambano lisilo la ubingwa.
“Mpambano huo utakuwa wa uzito wa Middle Kilo 72,  na kwa sasa ninaendelea kujifua ili niweze kuishinda mpambano huo,”anasema.
Anaongeza kuwa atacheza kwanza mapambano kadhaa ya kujipima uwezo na mabondia wa huko kabla baadaye ya kuanza kuwania ubingwa wa dunia unaotambuliwa na vyama vya WBC na WBA.
Akizungumzia hali ya mchezo huo hapa nchini, Kimondo anasema umekuwa ukishuka kutokana na mabondia wale wale kupigana kila siku sambamba na kutojitosa kuwania mataji makubwa.
Anasema mabondia wengi wamekuwa waoga wa kucheza na mabondia wengine ikiwemo yeye kwa kuhofu kupigwa na kupoteza heshima zao hali ambayo haiwasaii kitu katika medani hiyo.
“Kila siku ni Cheka (Francis), Nyilawila (Karama), Maugo (Mada), Kaseba (Japhet) hakuna wengine wapya, sasa hii haiwasidii kituy na inaonesha ni waoga wa kuthubutu kucheza na wengine, “anasema.
Kimondo anasema kwa kudhihirtisha kauli yake baadhi ya mabondia wamekuwa wakikwepa kuzipiga naye na kutoa visingizoi kibao yote nmi hofu ya kupigwa na kupoiteza sifa zao.
Akiwa na matarajio ya kufika mbali zaidi katika medani hiyo, Kimondo anawashauri mabondia wenzake kujituma kwa kufanya mazoezi ya kutosha badala ya kutafuta umaarufu kupitia  vyombo vya habari.
“Wasipigane kwa kuzoeaa , tunataka bingwa wa kweli na si bora bingwa,’anasema Kimondo.
Aidha, Kimondo anamshukuru mmiliki wa kampuni ya mabasi ya Sumry, Humud Mohammed Summry ambapo amekuwa akifanya kazi kama msimamizi na kusema kuwa bossi huyo amekuwa akimsaidia sana katika jitihada zake za kujiendeleza katika mchezo huo.


KIMONDO NI NANI:
Jina la kimondo lilitokana na uzito wa ngumi zake ambapo alipewa mwanzoni mwa miaka ya 2000 alipokipiga na Joseph Marwa katika moja ya pambano lililoandaliwa na kampuni ya Dynamite chini ya Shomary Kimbau.
Na aliitwa Kimondo baaada ya Sayari moja kuanguka mkoani Mbeya  ambapo ndipo asili ya Kimondo katika miaka ya 2000.
Akiwa ni mzaliwa wa Kyela mkoani  Mbeya,Kimondo alikuwa akiupenda mchezo huo tangua akiwa mdogo na hiyo inatokana na kuvutiwa na bondia bingwa wa zamani wa uzito wa juu duniani, Mike Tyson.
Baada ya kumaliza shule alijibidiisha katika kujifunza mchezo huo chini ya Mwalimu Jordan Mwanjelwa na kisha Omary Yazidu kabla ya kutua mikononi mwa Said Tambwe ambaye alimuzesha kuwa bondia mahiri.
Kimondo aliwahi kutwaa ubingwa wa Afrika Masharik na Katika mwaka 2011 kwa kumtwanga Mkenya Moses Odhiambo katika pambano la uzito wa Super Middle.
Aidha, Kimondo amewako kuzidunda na Fike Wilson, Rashid Matumla, MAneno Oswald ‘Mtambo wa Gongo’ na kutoshana nguvu, huku akimtandika Karama Nyilawila.
Maoni:dinazubeiry@gmail.com au tembelea http: dinaismail.blogspot.com

Comments