MALKIA WA NYUKI APASUA JIPU:ASEMA HAUNGI MKONO KUNDI LOLOTE KWANI AKILI YAKE NI KUIPATIA MAFANIKIO TIMU YA SIMBA
MAKAMU
Mwenyekiti wa kamati maalum ya kuisimamia klabu ya Simba, Rahma Al Kharoos ‘Malkia
wa Nyuki’ amesema hayuko tayari kufanya kazi na kundi lolote ndani ya klabu ya
Simba na kwamba akili yake ipo katika kuiwezesha timu ifanye vizuri kwenye
mechi zake za ligi ili iweze kupata nafasi za juu.
Al Kharoos
ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa kamati ya fedha ya Simba amelazimika kutoa
kauli hiyo kufuatia baadhi ya wanachama wa klabu hiyo kuung’oa uongozi wa klabu
hiyo chini ya mwenyekiti wake, Alhaj Ismail Aden Rage na kumteua yeye pamoja na
Zachari Hanspope kuongoza kwa muda.
Hata hivyo,
Hanspope ambaye alikuwa ni mjumbe wa kamati ya utendaji ya Simba kabla ya
kubwaga manyanga hivi karibuni, alikataa utezi huo na kusema anaheshimu katika
ya klabu hiyo.
Akizungumza
kwa simu leo kutoka nchini Uingereza, Al Kharoos alisema hayupo upande wowote
ndani ya klabu hiyo kwani uwepo wake Simba ni katika kuisaidia timu hiyo ifanye
vizuri katika kwenye michezo yake iliyosalia.
Alisema kwa
kuendeleza malumbano ambayo hayana tija na matokeo yake wanaweza kujikuta timu
inapotea zaidi kwenye ligi na mwisho wa siku wanakosa wa kumlaumu.
Aicha Al
Kharoos aliongeza kwa kitu muhimu kwake ni kuisaidia timu na si kuongoza na
kama uongozi utakuja baadaye, hivyo anachokingalia kwa sasa ni mustakabali
mzima wa timu hiyo.
“Sipo upande
wa harusi wala talaka mimi ninaangalia zaidi mafanikio ya timu nataka timu
iopande hadi nafasi ya pili na huwezi jua inaweza ikatokea miujiza na kushika
hata nafasi ya kwanza,”alisema
“Pamoja na
kuwa nipo safari ninamawasiliano ya karibu sana na benchji la ufundi ili kuwapa
hamasa katika utendaji wao...hapa akili zetu ni kushinda kwanza mechui zetu za
kule Kanda ya ziwa tukiuanza na Kagera Sugar na baadaye Toto African,”aliongeza
Alkharoos.
Comments
Post a Comment