KIKOSI cha Stars kilichopo
kambini kujindaa na mchezo huo kimekamilika baada ya wachezaji wake Mbwana
Samata, Thomas Ulimwengu na wengine kutoka Azam Fc kuripoti kambini.
Samata na Ulimwengu
wanaokipiga katika klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC)
walijiunga na wenzao jana jioni, huku wachezaji wengine wa Azam Fc John Bocco,
Mwadini Ally, Aishi Manula na Hamisi Mcha walijiunga jana.Wachezaji hao wote
walikuwa wakizichezea timu zao wikiendi iliyopita katika michuano ya
kimataifa.
Wambura alisema kwamba, Stars
inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium
Lager ikiwa chini ya Kocha Kim Poulsen inaendelea na mazoezi yake kwenye Uwanja wa
Taifa.
Comments
Post a Comment