LICHA ya kuchanua na ushindi
wa mabao 2-1 dhidi ya Barrack Young Controllers II ya Liberia , wawakilishji wa Tanzania kwenye
kombe la Shirikisho Barani Afrika Azam Fc, wamesema hawatabweteka na ushindi
huo.
Azam Fc ambayo ilirejea leo asubuhi kutoka Monrovia , Liberia
ambapo ilikwaana na wenyeji hao jumapili iliyopita.Wanatarajiwa kurudiana hapa
nchini kati ya Aprili 6 na 7 mwaka huu kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam .
Ofisa habari wa Azam Fc Jaffer Idd, aliiambia Sports Lady kwamba, pamoja na kushukuru kwa
ushindi huo alisema mchezo ulikuwa na ushindani mkubwa kwani wapinzani wao wako
vizuri huku timu ikiundwa na wachezaji
wengi vijana na wenye vipaji vya hali ya juu.
Alisema kutokana kiwango cha
hali ya juu walichokiona kwa wapinzani wao hawana budi kujipanga vizuri kwa
mechi ya marudiano ili kuhakikisha wanapata ushindi utakaowawezesha kusonga
mbele kwenye michuano hiyo.
“TUnashukuru tumerejea salama
nchini, kikubwa tutaendelea na maandalizi yetu kama
kawaida kwani tuna michezo ya Ligi Kuu ya Vodacom inatusubiri tukianza na
wikiendi hii na wiki ijayo kabla ya kujipanga zaidi kwa ajili ya mchezo wetu
huo na Waliberia”, Alisema Idd
Aidha, Idd amewashukuru
mashabiki wa timu hiyo kwa kutoa ushirikiano wa hali ya juu kwa kwa wengine
kwenda Liberia
kuishangilia timu hiyo hivyo kuwapa ari wachezaji ya kujituma zaidi uwanjani na
mwisho wa siku kuibuka na ushindi.
Azam Fc ambayo ni timu pekee
ya Tanzania
inayowakilisha kwenye michuano ya kimataifa ilikutana na Waliberia hao baada ya
kuondosha Al Nasr Juba Fc ya Sudan Kusini kwa jumla ya mabao 8-1.
Comments
Post a Comment