TIMU ya Simba, kesho inaanza
kampeni ya michuano ya kimataifa kwa kuwakaribisha mabingwa wa soka wa Angola ,
timu ya Recreativo de Libolo katika mechi ya kwanza ya hatua ya awali ya Ligi
ya Mabingwa Afrika.
Kocha mkuu wa Simba, Mfaransa Patrick
Liewig, alisema kikosi chake kipo imara na tayari kuanza vizuri
kampeni hiyo ya kimataifa
Alisema anashukuru wachezaji
wake kuwa wenye afya njema na ari kubwa kuelekea mechi hiyo, hivyo anaamini
watapata matokeo mazuri.
Liewig alisema pamoja na ugumu
wa mechi hiyo kutokana na ubora wa timu za Angola dimbani, lakini wamejipanga
kupata ushindi kujiweka nafasi nzuri kabla kurudiana.
“Vijana wangu wapo tayari
kuwakabili wapinzani wetu Libolo, wameahidi kucheza kwa juhudi kubwa ili
kushinda na kujiweka kwenye nafasi nzuri kabla ya kurudiana, tunaomba sapoti ya
Watanzania,” alisema.
Naye Jamhuri Kihwelo ‘Julio’
ambaye ni Kocha Msaidizi, amewasihi wapenzi na mashabiki wa soka kujitokeza na
kuishangilia Simba katika mechi ya kesho.
Comments
Post a Comment