Villa Squad na Moro United zinaumana kesho (Februari 2
mwaka huu) Uwanja wa Karume, Dar es
Salaam katika moja ya mechi za kundi B za Ligi Daraja
la Kwanza (FDL) inayoanza mzunguko wa lala salama.
Kundi A litakuwa na mechi kati ya Mbeya
City na Burkina Faso itakayochezwa Uwanja
wa Sokoine jijini Mbeya, Majimaji na Kurugenzi katika Uwanja wa Majimaji mjini
Songea, na Polisi Iringa dhidi ya Mkamba Rangers kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya
Samora mjini Iringa.
Mechi nyingine ya Kundi B itakuwa Transit Camp na
Ndanda itakayochezwa Uwanja wa Mabatini mkoani Pwani. Kundi C ni Polisi Dodoma
na Kanembwa JKT (Uwanja wa Jamhuri, Dodoma ),
Morani dhidi ya Mwadui (Uwanja wa Kiteto, Manyara), Polisi Mara na Pamba (Uwanja
wa Karume, Musoma), Polisi Tabora na Rhino Rangers (Uwanja wa Ali Hassan
Mwinyi, Tabora).
Ligi hiyo inatarajiwa kumalizika mwishoni mwa Machi mwaka
huu ambapo mshindi wa kila kundi atapanda daraja kucheza Ligi Kuu msimu ujao.
Comments
Post a Comment