KAMATI ya Uchaguzi ya
Shirikisho la soka Tanzania
(TFF), imesitisha uchaguzi mkuu wa Shirikisho hilo uliokuwa umepangwa kufanyika Februari
24, ili kurekebisha dosari za kikanuni zilizojitokeza.
Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Mwenyekiti wa Kamati hiyo,
Deogratius Lyato ilieleza kuwa , tarehe ya mpya ya uchaguzi huo itawekwa
wazi bada ya jambo hilo
kupatiwa ufumbuzi kwa nujibu wa taratubu zilizopo.
“Narudia tena, hakuna dosari
kwenye kanuni, isipokuwa ni matatizo madogo madogo yaliyojitokeza wakati wa
zoezi, hivyo si kwamb zoezi zima litaanza upya, hapana…litaendelea kuanzia
lilipofikia sasa,” alisema Lyatto.
Alisema kamati yake imefikua
uamuzi huo kwa mamlaka iliyopewa kwa mujibu wa kanuni kwani katika ibara ya
10(5), kamati yake inaruhusiwa kupangua, kubadilisha tarehe, kusimamisha au
kusitisha kabisa zoezi la uchaguzi.
Lyato alisema uamuzi huo
ulifikiwa na kamati yake katika kikao kilichofanyika mwishoni mwa wiki ambapo
pamoja na mambo mengine, walijadili pia mchakato wa uchaguzi huo kutokana na
hali iliyojitokeza.
Alisema kusitishwa kwa
uchaguzi huo wa TFF kunakwenda sambamba na ule wa uchaguzi huo wa Bodi ya Ligi
Kuu iliokuwa ufanyike Februari 22.
Aidha, Lyato jana alijikuta
kwenye wakati mgumu pale alipotakiwa kutoa ufafanuzi wa kikanuni juu ya mdau
Agape Fue aliyekuwa amempinga Jamal Malinzi ambaye pingamizi lake lilitupwa
na kamati yake kwa kukosa sifa, lakini
likaibukia Kamati ya Rufaa ya Idd Mtiginjola.
Akijibu swali hilo , Lyato alisema mdau
huyo Agape Fue ana haki kwa kuwa alifuata kanuni ya ibara 12 (1 na 2) ya
uchaguzi ambacho kinairuhusu Kamati ya Rufaa kusikiliza ombi la mtu ambaye
hajaridhishwa na maamuzi ya Kamati yake.
Comments
Post a Comment