SHIRIKISHO
la Soka Tanzania (TFF) limezitaka timu za Azam Fc na Simba kuutumia vema
uenyeji wake kwa kuhakikisha zinashinda mechi zake za kimataifa zitakazopiugwa
mwishoni mwa wiki hii.
Wakati
Azam Fc itashuka jumamosi kwenye uwanja wa Taifa kuikabili Al Nasri Juba Sudani
Kusini katika kombe la Shirikisho, Simba itashuka jumapili kwenye uwanja huo
kuivaa Recretivo de Libolo ya Angola katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika.
Katibu
Mkuu wa TFF, Angetile Osiah amesema leo kwamba anaamini Azam na Simba
zimejipanga vema kwa mechi hizo ambazo zitakuwa na uopinzani mkubwa kwani timu
wanazokutana nazo zinatoka ukanda wenye upinzani.
“Juba
inashiriki kwa mara ya kwanza michuano ya kimataifa baada ya nchi yao kupata
uanachama wa FIFA mwaka jana na nnaamini watakuwa wamejipanga, hata hawa
wapinzani wa Simba si timu ya kubeza pia hivyo Simba nayo ina mtihani
mkubwa,”alisema
Aidha,
Osiah aliwataka mashabiki wa soka nchini kuacha siasa za Usimba na Uyanga kwa
kuzomea uwanjani wakati timu hizo zitakapoishuka badala yake kuungana pamoja
kuzishangilia ili kuwapa nguvu wachezaji.
“Hizi
timu ni za Tanzania kama zitashinda sifa itakuja kwa Tanzania na kama
zitashindwa aibu itakuja kwa Tanzania na si timu, hivyo nawaomba mashabiki
tuache tabia za kuzomea hovyo uwanjani,’alisema
Aidha,
Osiah amewaomba viongozi wa timu za Azam na Simba kutotengeneza mazingira ya
kihasama kwa timu opinzani badala yake kuzipa ushirikiano wa kutosha tangu
zinapotua nchini hadi kuondoka kwake baada ya mechi.
Comments
Post a Comment