Skip to main content

TENGA AONGEZA WAWILI KAMATI YA NIDHAMU


Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga ameteua wajumbe wawili kuingia kwenye Kamati ya Nidhamu ya TFF baada ya nafasi mbili kuwa wazi kutokana na mmoja kuteuliwa kuongoza kamati nyingine ya TFF na mwingine kufariki dunia.

Iddi Mtiginjolla ambaye alikuwa mjumbe wa Kamati ya Nidhamu hivi karibuni aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF baada ya Shirikisho kufanya mabadiliko ya katiba yaliyotokana na maagizo ya Shirikisho la Kimataifa la Vyama vya Mpira wa Miguu (FIFA), wakati mjumbe mwingine wa Kamati ya Nidhamu, Shaaban Semlangwa alifariki dunia katikati ya mwaka uliopita. 
Wajumbe wapya walioteuliwa ni Jesse Mguto- alikuwa Hakimu Mkazi na kwa sasa ni mwanasheria na Wakili wa Mahakama Kuu. Ana Digrii ya Sheria. Mwingine ni Yohane Masala ambaye kwa sasa ni Mwanasheria Mwandamizi wa Serikali (Principal State Attorney). Ana Digrii ya Kwanza na ya Pili ya Sheria na Digrii ya Pili katika masuala ya Amani na Haki (MA in Peace and Justice).

Rais Tenga amesema ana imani na uwezo wa watu hao na kwamba watafanya kazi yao kwa uadilifu ili Shirikisho liendelee kuboresha utawala bora.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Comments