WAKATI
kikosi cha Simba kinatarajiwa kuwasili kesho kutoka Arusha kilipokuwa kimepiga
kambi, kiingilio cha chini cha mchezo wake wa ligi ya mabingwa dhidi ya
Recretivo de Libolo ya angola kimepangwa kuwa sh.5,000.
Timu hizo
zinatarajiwa kukwaana jumapili kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam
ambapo kiingilio hicho kitahusisha mashabiki watakaokaa viti vya rangi ya
kijani na bluu.
Ofisa habri
wa Simba Ezekiel Kamwaga alisema kwamba kikosi cha timu hiyo mara baada ya kurejea
Dar es Salam leo kitaingia kambini kwenye hoteli ya Spice iliyopo katika ya
jiji kuendelea na maandalizi yake.
Alisema
wachezaji wote ukiacha majeruhi Felix Sunzu na Paul Ngalemwa wao majeruhi, wapo
katika hali nzuri na jana asubuhi walifanya mazoezi ya mwisho huku jioni
wakipewa mapumziko.
Kamwaga
aliongeza kuwa kwa sasa kikosi kipo tayari kwa mchezo huo unaotarajiwa kuwa na
ushindani mkubwa na hasa ikizingatiwa kuwa wapinzani wao nao wamejipanga vema,
lakini watahakikisha wanashinda.
Aidha,
Kamwaga alivitaja viingilio vingine ni sh 10,000 kwa watakjaokaa viti vya rangi
ya chungwa, sh 15,000 kwa watakaokaa VIP C, sh 20,000 kwa VIP B na sh 30, kwa
VIP A.
Comments
Post a Comment