KAMATI ya utendaji ya klabu ya Simba imeazimia kuitisha
mkutanio mkuu wa dharura wa klabu hiyo ambao utakuwa na ajenda moja tu ya
kujadili mwenendo mbaya wa klabu hiyo kwenye ligi kuu ya Vodacom.
Ofisa habari wa
Simba Ezekiel Kamwaga amesema leo kwamba kamati ya utendaji ya Simba iliyokutana
jana usiku imepitisha uamuzi wa kuitishwa kwa mkutano huo ili kujadili hali
hiyo.
Alisema wanatarajiwa kutangaza tarehe na mahala
utakapofanyika mkutano huo wakati wowote kuanzia sasa na kwamba uongozi
umewataka wanachama wa klabu hiyo kusuusubiria mkutano huo.
“Uongozi pia umesikitishwa na sintofahamu inayoendelea ndani
ya klabu yetu na hasa katika michezo yake ya ligi kuu hivyo basi uongozi umekubaliana kuitisha mkutano mkuu wa
dharula ili kuweza kutafuta ufumbuzi wa hali hii,”alisema.
Comments
Post a Comment