Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linatoa pongezi
kwa uongozi mpya wa Chama cha Wachezaji Mpira wa Miguu Tanzania (SPUTANZA) na
wa Chama cha Waamuzi wa Mpira wa Miguu Tanzania (FRAT) uliochaguliwa wiki
iliyopita.
Uongozi wa FRAT ulichaguliwa Februari 13 mwaka huu mjini
Morogoro wakati wa SPUTANZA ulichaguliwa jana (Februari 17 mwaka huu) katika
uchaguzi uliofanyika Kigamboni, Dar es
Salaam .
Waliochaguliwa kuongoza SPUTANZA na hawakuwa na wapinzani ni
Musa Kissoky (Mwenyekiti) na Said George (Katibu Mkuu) wakati Ali Mayai
aliwashinda Isaac Mwakatika na Hakim Byemba katika nafasi ya mjumbe wa Mkutano
Mkuu wa TFF.
Kusianga Kiata na Charles Mngodo walichaguliwa kuwa wajumbe
wa Kamati ya Utendaji ya SPUTANZA. Katika uchaguzi huo uliohudhuriwa na wapiga
kura 17, Mhazini na nafasi moja ya mjumbe wa Kamati ya Utendaji zitajazwa
baadaye kutokana na kukosa wagombea.
Kwa upande wa FRAT viongozi waliochaguliwa ni Said Nassoro
(Mwenyekiti), Charles Ndagala (Katibu Mkuu) na Kamwanga Tambwe (mjumbe wa
Mkutano Mkuu wa TFF).
Ushindi waliopata viongozi waliochaguliwa kuongoza vyama
hivyo unaonesha jinsi wapiga kura walivyo na imani kubwa kwao, na TFF inaahidi
kuendeleza ushirikiano wake kwa Kamati ya Utendaji ya FRAT na SPUTANZA.
Uongozi huo mpya una changamoto nyingi, kubwa ikiwa ni
kuhakikisha unaendesha shughuli za mpira wa miguu kwa kuzingatia katiba zao
pamoja na vyombo vya mpira wa miguu vilivyo juu yao .
Pia tunatoa pongezi kwa kamati za uchaguzi za FRAT na
SPUTANZA na Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa kuhakikisha uchaguzi umeendeshwa kwa
mujibu wa Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF.
Comments
Post a Comment