KIKOSI cha kosi cha timu hiyo kinatarajiwa kuondoka Ijumaa alfajiri
kuelekea Luanda , Angola kwa ajili ya mchezo wake wa
klabu bingwa ya Afrika dhidi ya wenyeji Recreativo do Libolo ya huko utakaopigwa
jumapili katika mji wa Calulo nchini humo.
Kikosi cha wachezaji 20 na viongozi saba wa Simba
wakiongozwa na mwenyekitii wa kamati ya usajili ya Simba, Zacharia Hanspoppe
pamoja na mjumbe wa kamati ya utendaji ya Shirikisho la soka Tanzania (TFF)
Mohsin Balhabou ndicho kitakachokwenda Angola .
Hata hivyo Kamwaga alisema awali mchezo huo ambao ulikuwa
upigwe jumamosi mjini Luanda sasa utapigwa jumapili mjini Caculo ambapo umbali
kutoa Luanda hadi Caculo ni masaa manne,hivyo wameandika barua kwa wenyeji wao
kuomba wapatiwe usafiri wa ndege kwa mujibu wa sheria na kanuni za Shirikisho
la Soka Afrika (CAF).
Comments
Post a Comment