Baadhi ya mashabiki na wanachama wa Simba na Yanga wakizungumza na waandishi wa habari leo kuhusiana na hatua watakazozichua baada ya kuenguliwa katika kinyang'aro cha uchaguzi wa TFF, Jamal Malinzi.Kutoka kushoto ni Salum Mkemi, Suleiman Kato an Kaisi Edwin.
WANACHAMA
na mashabiki wa soka nchini wameapa
kuandamana na kwenda mahakamani kuzuia kufanyika kwa uchaguzi wa viongozi wa
Shirikisho la soka Tanzania (TFF), baada ya kamati ya Rufaa ya Shirikisho hilo
kumuengua mgombea wa nafasi ya urais, Jamal Emil Malinzi.
Aidha,
wanachama hao kutoka vilabu vya Simba, Yanga na Azam wamemtaka Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete kuingilia kati suala la
kuenguliwa kwa Malinzi kwani limefanywa kwa chuki binafsi likiwa na lengo la
kumbemba mpinzani wake, Athuman SIKU moja baada ya kamati Nyamlani.
Wakizungumza
na waandishi wa habari leo, pamoja na kupinga kuondolewa kwa Malinzi, wametoa siku tatu kwa TFF kumrejesha katika kinyang’anyiro hicho, kinyume na hapo
watakwenda kudai haki yao mahakamani.
Mmoja
ya wadau hao Kaisi Edwin alisema kwamba kanuni za Shirikisho la Soka la
Kimataifa (FIFA) chombo cha mwisho cha maamuzi ni Mahakama yas Usuluhishi wa
Migogoro ya Michezo (CAS) lakini TFF haijaelekeza baada ya kamati ya Rufaa
chombo kipi kinaweza kutoa suluhu ya masuala kama hayo.
Alisema
walitaka kupata changamoto mpya ya uongozi kupitia kwa Malinzi lakiini kitendo
cha kumuengua kunaonesha ni jinsi gani wanavyotaka kuendelea kuwa na watu
wasiotaka maendeleo ya soka.
“Ni
bora tufungiwe na FIFA, tunajua maslahi wanayoyapata TFF na tutatoa uozo
wote...kwa hili hata damu itamwagika na kwa gharama yoyote tutahakikisha
uchaguzi haufanyiki kama wasipomrejesha Malinzi labda waende kufanyia
Geneva,”aliusema Kaisi.
Naye
Suleiman Kato alisema anashangazwa na kamati ya Rufaa kumuengua Malinzi kwa
madai ya kutokuwa na uzoezfu wakati alipitishwa kugombea uchaguzi wa mwaka 2008
inagawa alishindwa kwa kura chache na rais wa sasa wa TFF, Leodger Tenga.
“Malinzi
pia nia mwenyekiti wa chama cha soka Kagera sasa iweje apitishe kugombea huko
na mpaka anapata kiti hicho nah ii leo mseme hana uzoefu na uongozi wa
soka, kinachoonekana hapa ni kutaka kudidimiza soka la Tanzania, hilo
hatulikubali,”alisema.
Mdau
mwingine, Mgeni Ramadhan ‘Dogo Macho’ alisema inaonesha wazi wazi wanataka
viongozi kwa ajili ya maslahi binafsi kitu ambacho si sahihi kwani Watanzania
wanaopenda soka wanataka maendeleo na si viongozi maslahi.
“Naamini
Rais kikwete ambaye ni mpenda michezo atasikia kilio hiki na kuingilia kati,
kuna watu wapo kwa ajili ya kubebwa, huyo Nyamlani anatoka Kusini, kuna
mwanakamati mmoja Murtaza mangungu ambaye ni Mbunge anambeba, pia kuna mwingine
aliwahi kuwa Hakimu wa Temeke na nyamlani akiwa karani wake,”alisema.
Kwa
upande wake, mdau mwingine Said Bakari alisema kuwa wataanza kuonesha hasira
zao kuanzia leo kwenye uwanja wa Taifa kwenye mechi baina ya Yanga na African
Lyon, kabla ya kuendelea na hatua yao katika michezo ya kimataifa ya timu za
Simba na Azam wikiendi hii.
“Huyu
malinzi anabebwa kwani tunajua mwenyekiti wa kamati alikuwa wakati akiwa Hakimu
temeke yeyealikuwa karani, Mangungu naye pamoja na kumpigia debe ni jirani na
baba yake Nyamlkani,”alisema.
Wadau
hao kwa pamoja wamepaza sauti hizo baada kamati ya Rufaa ya TFF kumuengua
Malinzi katika uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika februari 24 mwaka huu ambapo
kwa mujibu wa ratiba kampeni zinatarajiwa kuanza leo.
Katika
hatua nyingine, Malinzi kesho anatarajiwa kuzungumza na waandishi wa habari
kuhusiana na sakata hilo.
Comments
Post a Comment