Baadhi ya makamishna wa VPL na FDL wameondolewa na wengine
kusimamishwa kusimamia mechi za ligi hizo kutokana na upungufu kwenye ripoti
zao au kutowasilisha kabisa ripoti hizo TFF baada ya mechi.
Kamishna Mohamed Jumbe aliyesimamia mechi kati ya Mgambo
Shooting na Simba ameondolewa kwenye orodha ya makamishna kutokana na ripoti
yake kuwa na upungufu.
Makamishna wa mechi kati ya JKT Oljoro vs Yanga (Hakim
Byemba), JKT Oljoro vs Kagera Sugar (Salum Kikwamba), Toto Africans vs African
Lyon (Charles Komba), Coastal Union vs JKT Oljoro (Mohamed Nyange)
wamesimamishwa hadi watakapowasilisha ripoti zao TFF.
Kwa upande wa FDL makamishna waliosimamishwa hadi
watakapowasilisha ripoti zao TFF ni wa mechi kati ya Kurugenzi vs Polisi
Iringa, Morani vs Mwadui, Polisi Mara vs Pamba, Polisi Mara vs Mwadui, Morani
vs JKT Kanembwa na Pamba vs Polisi Dodoma.
Wengine ni Mwadui vs JKT Kanembwa, Polisi Tabora vs Morani,
Polisi Dodoma vs Polisi Mara, Polisi Tabora vs Mwadui, Polisi Mara vs Morani,
JKT Kanembwa vs Polisi Mara, Morani vs Rhino Rangers na Small Kids vs Mkamba
Rangers.
Kamati ya Ligi imewakumbusha makamishna wote kuwa ni jukumu
lao kuhakikisha ripoti zao zimefika TFF na kurekebisha upungufu wa jinsi ya
kuripoti matukio yanayotokea uwanjani. Licha ya kutuma nakala kwa njia ya
email, wanatakiwa pia kuwasilisha ripoti halisi (original) TFF.
Comments
Post a Comment