KUMBUKUMBU


Mzee Mbonea Kazeni Mshana.
Leo ni miaka 10 tangu ulipochukuliwa kukaa na Baba yetu wa Mbinguni Milele Tarehe 1/02/2003. Tunakumbuka, busara, hekima, kujali, malezi bora ya kwako uliyotupa. Tunakumbuka bidii, juhudi na uchapa kazi wako. Lakini tunaamini kuwa umepumzika na taabu za dunia hii vizuri.
Unakumbukwa na mkeo mpendwa Rahel Mshana, Wanao wapendwa Joyce, Felix, Joseph, Judith na Brian, pia wakwe zako Godlisten, Stephen na Neema na wajukuu zako Innocent, Rachel, Sarah, Daniel, Gideon, Elisha, Reinhard, Rachel na Jonathan.
Pia unakumbukwa na mkweo Naizihijwa Joseph Mritha, na Ndugu Zako na jamaa na marafiki tulioishi nao kwa upendo Mwadui -Shinyanga na Arusha.
Ufunuo 14: 13...."Heri wafu wafao katika Bwana Tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao"

Comments