KILA LA HERI, SIMBA, AZAM & JAMHURI


Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linazitakia kila la kheri timu za Azam, Jamhuri na Simba ambazo zinaiwakilisha Tanzania katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho. 
Azam inacheza na Al Nasir Juba ya Sudan Kusini katika mchezo wa Kombe la Shirikisho utakaofanyika Jumamosi (Februari 16 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. 
Nayo Jamhuri ya Zanzibar kesho itacheza na St. Georges ya Ethiopia katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika utakaofanyika Uwanja wa Gombani kisiwani Pemba. Simba itacheza na Recreativo do Libolo ya Angola keshokutwa (Februari 17 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Comments