Mwenyekiti wa simba, Ismail Aden Rage pamoja na mfadhili wa timu hiyo, Rahma Alkharoos wakinesha moja ya jezi watakazopewa na tim,u ya Sunderland ya Uingereza kama sehemu ya ufadhili wao.
WACHEZAJI chipukizi wa timu ya soka ya Simba Ramadhan
Singano ‘Messi’ na Shomari Kapombe wanatarajiwa kwenda kufanya majaribio katika
kituo maalum cha vijana cha klabu inayoshiriki Ligi Kuu ya England, Sunderland.
Aidha, viongozi wa Simba, wanatarajiwa kwenda huko hivi
karibuni ambapo pamoja na mambo mengine
watashuhudia mechi ya ligi kuu ya England baina ya wenyeji Sunderland dhidi ya
Fulham itakayopigwa Machi 2 mwaka huu.
Mwenyekiti wa Simba
Alhaj Ismail Aden Rage alisema, hatua hiyo inafuatia ushirikiano baina yao na
Sunderland uliotokana na matunda ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Jakaya Kikwete.
Alisema katika makubaliano yao ya ushirikiano na udhamini,
Sunderland ambayo imepania zaidi kuwekeza katika soka la vijana ambapo itakuwa
ikichukua wachezaji katika makundi tofauti ya umri wa klabu ya Simba na kwenda
kujifunza katika taasisi yao ya vijana.
Rage aliongeza kuwa, Kapombe na Singano watakwenda huko mara
baada ya kumalizika kwa ligi kuu ya Vodacom ambapo pamoja na kupatiwa mafunzo
maalum katika kituo cha kulea vijana cha timu hiyo, kama watafanya vema katika
mazoezi yao huenda wakasajiliwa kuichezea timu ya vijana ya Sunderland.
Aidha, Rage aliongeza kuwa mazungumzo kuhusiana na udhamini
wao na Sunderland yapo katika hali na ndiyo maana uongozi umealikwa kwenda huko
si kwa ajili tu ya kushuhudia mechi bali kubadiklishana uzoefu na viongozi wa
timu hiyo.
Comments
Post a Comment