Skip to main content

FDL KUENDELEA KUTIMUA VUMBI WIKIENDI


Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kuwania tiketi za kucheza Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu ujao inaendelea kutimua vumbi wikiendi hii kwa mechi kumi na moja zitakazopigwa kwenye viwanja mbalimbali.

Kundi A keshokutwa (Februari 10 mwaka huu) Mbeya City itacheza na Polisi Iringa katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya, Mkamba Rangers itaumana na Burkina Faso (Uwanja wa CCM Mkamba) wakati JKT Mlale itakuwa mwenyeji wa Kurugenzi kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea.

Green Warriors na Ndanda zitacheza kesho (Februari 9 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Karume, Dar es Salaam katika moja ya mechi za kundi B. Mechi nyingine kundi hilo kesho ni kati ya Tessema na Villa Squad kwenye Uwanja wa Mabatini mjini Mlandizi.

Keshokutwa (Februari 10 mwaka huu) Transit Camp itacheza na Ashanti United kwenye Uwanja wa Karume, Dar es Salaam wakati Polisi Dar es Salaam na Moro United zitavaana Uwanja wa Mabatini mjini Mlandizi.

Kundi C kesho (Februari 9 mwaka huu) ni Polisi Dodoma vs Polisi Tabora (Uwanja wa Jamhuri, Dodoma), Polisi Mara vs Mwadui (Uwanja wa Karume, Musoma), Morani vs Kanembwa JKT (Uwanja wa Kiteto, Manyara) na Rhino Rangers vs Pamba (Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora).

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Comments