WAKATI timu za soka za Tanzania ‘Taifa Stars’ na ile ya
Cameroon ‘Indomitable Lions’ zinashuka leo katika uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam, makocha wa timu hizo Mdenmark Kim poulsen wa Stars na Mfaransa Jean
Paul Akono wametamba vikosi vyao kuibuka na ushindi.
Timu hizo zitakutana katika mchezo wa kimataifa uliopo
kwenye kalenda ya Shirikisho la Soka Kimatifa (FIFA), utatumika kama
maandalizxi kwa timu hizo kwa ajili ya kujiandaa na mechi zake za kuwania tiketi ya kucheza
fainali ya kombe la Dunia zitakazopigwa mwakani nchini Brazil.
Wakati Stars itasaka tiketi ya kombe la Dunia kwa kucheza na
Morocco, Machi 24 mwaka huu Uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam, Cameroon inatarajiwa kukwaana na Togo.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Poulsen pamoja na kufurahi kupata nafasi ya
kucheza na Cameroon kutokana, alisema kwamba kikosi chake kipo tayari kwa
mchezo huo ambao ni muhimu kwao kwani utawasaidia sana katika maandalizi yao ya
kuivaa Morocco.
Alisema amekuwa akihitaji
mechi ngumu kama hiyo ili kujenga timu imara na kwamba amekiandaa vema kikosi
chake kupitia mazoezi ya siku chache walizokaa kambini na kwa ari pamoja na
utayari walionao vijana wake anaimani watafanya vema katika mchezo huo.
“Napenda sana
kaulimbiu ya Umoja ni nguvu, wachezaji ni wamoja, sisi wote ni wamoja na hivyo
wachezaji wangu wanatakiwa kucheza vizuri mchezo huu ili kuwapa changamoto
Cameroon na hasa ikizingatiwa kuwa watanzania wanasubiri mambo mazuri kutoka kwao,”alisema
Kocha huyo aliongeza kuwa anaiheshjimu Cameroon kwani ni
timu nzuri na yenye wachezaji wazuri lakini hilo haliwazuiii kushinda mchezo wa
leo huku wakiamini mtindo wao wa uchezaji ni kupiga pasi kwa wingi na
kutengeneza nafasi na kufunga, huku wakicheza
kwa haraka na hata wakipoteza mpir wanajituma wote kuutafuta.
Naye nahodha wa Stars, Kaseja alisema kwamba wako tayari kwa
mchezo huo, kinachohitajika zaidi ni umoja baiina yao ili kuweza kushinda,
hivyo amewaomba Watanzania kujitokeza kwa wingi uwanjani ili kuwaunga mkono.
Kwa upande wa kocha wa Cameroon, Akono pamoja na kufurahi
kupata nafasi ya kucheza na Stars alisema kikosi chake kiopo tayari kwa mchezo
huo ambao anaamini utakuwa na ushindani mkubwa kwani Stars pia ni timu nzuri.
Alisema mchezo wa leo si muhimu kwa Stars tu bali hata kwa
timu yake ambayo pia itakuwa na kibarua cha jkucheza mechi ya kusaka kucheza
fainali za kombe la Dunia mwakani hivyo anaamini kila timu itacheza kwa nafasi
na uwezo ilionao ili mwisho wasiku itoke na matokeo mazuri.
Naye nahodha wa Cameroon, Pierre Wome alisema wamefurahi
kuja kucheza na Stars na kwamba wachezaji wenzake wapo tayari kwa mchezo wa leo
ambao utakuwa wa mwisho kwao katika maandalizi yao dhidi ya Togo mwezi Machi.
Kikosi cha Stars kilichopo kwenye hoteli ya Tansoma
kinaundwa ,makipa Juma Kaseja (Simba), Mwadini Ali (Azam) na Aishi Manula
(Azam). Mabeki ni Erasto Nyoni (Azam), Nassoro Cholo (Simba) ambaye ni majeruhi
, Aggrey Morris (Azam), Nadir Haroub (Yanga), Kelvin Yondani (Yanga), Shomari
Kapombe (Simba) na Issa Rashid (Mtibwa Sugar).
Viungo ni Amri Kiemba (Simba), Simon Msuva (Yanga), Frank
Domayo (Yanga), Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), Salum Abubakar (Azam), Khamis
Mcha (Azam), Athuman Idd (Yanga) na Mwinyi Kazimoto (Simba). Washambuliaji ni
Mrisho Ngasa (Simba), na Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wanaochezea timu ya
TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC).
Aidha kikosi cha Cameron kitawakosa nahodha wake Samuel Eto'oo Fills na Alexndre Song walio majeruhi hivyo kitawakilishwa na Herve Tchami wa Budapest Honved ya Hungary, beki
Nicolas Nkoulou wa Marseille ya Ufaransa, mshambualiji Jean Paul Yontcha wa SC
Olhanense ya Ureno, beki Jean Kana Biyick wa Rennes ya Ufaransa, mshambuliaji
Fabrice Olinga wa Malaga FC ya Hispania, beki Allan Nyom wa Udinese ya Italia
ambaye yuko kwa mkopo Granada ya Hispania na beki wa kushoto Henri Bedimo wa
Montpellier ya Ufaransa.
Wengine ni Charles Itandje, Benoit Assou Ekoto, Jehu Rustand
Youthe (Union Douala), Fabrice Olinga Essono, Allam Nyam, Bouba Aminou, Benoit
Angwa, Herve Tchami, Henri Bedimo, Nicolas Nkoulou, Jean Makoun, Jean Kana
Biyick, Joel Matip, Vincent Aboubakar, Alexandre Song, landre Nguemo, Pierre Wome, Jean Nyontcha, Achille
Emana na Charles Eloundou..
Viingilio katika mchezo huo utakaoanza saa 11 jioni sh 5,000
kwa viti vya kijani, sh 7,000 kwa viti vya bluu sh 10,000 kwa viti vya rangi ya
chungwa, sh 15,000 kwa VIP C, sh 20,000 kwa VIP B n ash 30,000 kwa VIP A.
Comments
Post a Comment