Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limesitisha
ukamishna wa Hafidh Ali. Uamuzi huo umefanywa na Kamati ya Mashindano ya Kombe
la Mataifa ya Afrika iliyokutana Januari 17 mwaka huu jijini Johannesburg,
Afrika Kusini.
Kwa mujibu wa barua ya Katibu Mkuu wa CAF, Hicham El Amrani
kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), ukamishna huo umesitishwa kwa
vile hadi sasa Shirikisho hilo halijapata ripoti ya mechi namba 78 kati ya
Comoro na Libya ambayo Ali aliteuliwa kuisimamia.
Hivyo, ukamishna wa Ali umesitishwa hadi hapo CAF
itakapopokea ripoti kuhusiana na mechi hiyo ambayo ilikuwa ni kutafuta tiketi
ya kucheza Fainali za AFCON zilizofanyika mwaka huu nchini Afrika Kusini.
Comments
Post a Comment