AZAM FC KIWANGO, YAITUNGUA AL NASR 1


TIMU ya Azam FC, imeanza vema kampeni ya michuano
ya kimataifa kwa ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya
Al Nasr Juba ya Sudan Kusini, mechi iliyopigwa
kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Ushindi huo sio tu faraja kwa wapenzi na mashabiki wa timu hiyo, bali kwa Watanzania hasa ikizingatia ndio mara ya kwanza kucheza michuano ya kimataifa.
Azam Fc ilikuwa ya kwanza kupata bao katika dakika ya 14, likifungwa na Abdi Kassim ‘Babi.’
Al Nasri walisawazisha dakika ya 39, likifungwa na Fabian Elias kutokana mpira wa krosi ya  Kone James.
Katika mechi hiyo iliyochezeshwa na mwamuzi Davies Omweno wa Kenya, mashabiki wa Yanga walishangilia Al Nasir na kuwakebehi watani zao Simba kuelekea mechi ya leo dhidi ya Libolo ya Angola.
Azam walionekana kuja na nguvu zaidi katika kipindi cha pili kwani dakika ya 80, Kipre Tche akaifungia bao la pili akiunganisha krosi ya Hamis Mcha aliyekuwa mwiba.
Tcheche alirejea kwenye nyavu za Al Nasr na kuifungia timu yake bao la tatu, hivyo kufanya kuvuna ushindi wa mabao 3-1.

Comments