WAKATI kikosi cha timu ya
Taifa ‘Taifa Stars’ kikitarajiwa kuondoka alasiri ya kesho kwenda Ethiopia , Yanga imeruhusu nyota
wake wawili kati ya watano walioitwa kwenye kikosi hicho.
Yanga ambayo imepiga kambi ya
maandalizi nchini Uturuki ilizuia nyota wake kujiunga na kambi ya Stars
iliyoanza jumapili iliyopita jijini Dar es Salaam
kujiandaa na mchezo huo utakaopigwa keshokutwa katika uwanja wa Taifa wa Addis Ababa .
Ofisa
habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Boniface Wambura ameiambia Sports Lady kwamba baada ya mazungumzo baina ya kocha mkuu wa Stars Kim Poulsen na yule wa Yanga
Ernie Brandts, walikubaliana beki Kelvin Yondan na Kiungo Frank Domayo wa Yanga
ndio wajiunge na Stars.
Yondan na Domayo wanatarajiwa kuwasili nchini usiku wa leo na endapo watachelewa watakwenda Ethiopia peke yao.Wachezaji wengine wa Yanga walioitwa Stars ambao wataendelea kubaki nchini
Uturuki ni pamoja na Athuman Iddy ‘Chuji’, Simon Msuva na Nadir Haroub ‘Cannavaro’
watakaojiunga na Stars watakaporejea nchini Januari 13 kutoka Uturuki.
Mchezo huo ni maalum kwa kuipa maandalizi ya mwisho Ethiopia kabla ya kwenda Afrika
Kusini kwenye fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) zitakazoanza
Januari 19 mwaka huu.
Aidha, Wambura aliongeza
kuwa, tayari wachezaji wa Simba, Azam Fc
na Mtibwa Sugar waliokuwa Zanzibar
na timu zao zinazoshiriki michuano ya kombe la Mapinduzi inayoendelea Visiwani Zanzibar
waliwasili mchana wa leo na kuungana na wenzao.
“Hata hivyo Azam Fc imeruhusu kipa mmoja tu Aishi Manula huku
Mwadini Ally ambaye pia aliitwa Stars ataendelea kubaki na timu kwenye kombe la
Mapinduzi,”alisema Wambura
Aliwataja wengine wachezaji
waliopo ni pamoja na Juma Kaseja kutoka Simba ambaye pia ndiye nahodha wa Stars
na Manula ( Azam FC), huku kwa upande wa
Mabeki ni Aggrey Morris (Azam), Amir Maftah (Simba), Erasto Nyoni (Azam), Issa
Rashid (Mtibwa Sugar), na Shomari Kapombe (Simba).
Viungo ni Salum Abubakar
(Azam), Amri Kiemba (Simba), Khamis Mcha (Azam), Mwinyi Kazimoto (Simba) na
Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), wakati washambuliaji ni Mbwana Samata, Thomas
Ulimwengu (TP Mazembe, Jamhuri ya
Kidemokrasi ya Congo- DRC) na Mrisho
Ngasa (Simba).
Stars ambayo pia itautumia
mchezo huo kama sehemu ya maandalizi ya mechi ya mchujo dhidi ya Morocco kuwania
tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia 2014, mchezo utakaochezwa Machi
mwaka huu.
Katika maandalizi yake hayo, mara
ya mwisho Stars ilikwaana na Zambia Desembza
22 mwaka jana kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na kuibanjua bao 1-0 katika mchezo wa kirafiki .
Comments
Post a Comment