YANGA YAONESHA ILICHOKIVUNA UTURUKI, YAWAPIGA WASAOTH 3-2


 Wachezaji wa Yanga wakishangilia
 Kikosi  cha YAnga

Kikosi cha Black Leopards




MABINGWA wa soka Afrika Mashariki na Kati, Yanga, leo wam evuna ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Black Leopards ya Afrika Kusini katika mechi ya kirafiki ya kimataifa iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Yanga wakicheza mechi ya kwanza tangu warejee nchini wakitokea Uturuki walikokuwa wamepiga kambi ya wiki mbili kujiandaa na raundi ya pili ya Ligi Kuu Bara, walionesha kiwango cha kuvutia hasa kipindi cha kwanza huku Jerry Tegete ‘Mturuki,’ Simon  Msuva na Haruna Niyonzima waking’ara zaidi.
Tegete alikuwa wa kwanza kuwainua katika viti mashabiki wa Yanga baada ya kuifungia bao kwa mkwaju wa penalti dakika ya 30, iliyotolewa na mwamuzi Hashimu Abdallah baada ya Niyonzima kuangushwa na beki Humphrey Khoza wa Leopards.
Katika kipindi cha kwanza,  Yanga walitawala kwa kiasi kikubwa huku Frank Domayo na Athumani Idd ‘Chuji’ wakikamata vema dimba huku Edger Manaka wa Leopards kumpunguza kasi Domayo kwa kumchezea rafu za mara kwa mara.
Dakika ya 13, nusura Yanga wapate bao kwa mpira uliotokana na free kick iliyopigwa na Joshua na kwenda nje sentimita chache langoni mwa Leopards, hivyo hadi timu hizo zinakwenda mapumziko, Yanga walikuwa mbele kwa bao 1-0.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi kwa timu zote kufanya mabadiko kadhaa na kusaka mabao zaidi, hivyo dakika ya 46, Khoza aliisawazishia timu yake bao kwa kichwa akiunganisha mpira wa kona uliokuwa umepigwa na Rodney Ramagalela.
Mabadiliko ya nyota wawili kila upannde mwanzoni mwa kipindi cha pili yalionekana kuidhoofisha Yanga huku Leopards wakionekana kucheza soka ya kutulia zaidi. Katika mabadiliko hayo, Yanga iliwatoa mapacha Kabange na Mbuyu Twite na kuingiza Simon Msuva na Juma Abdul.
Wageni Leopards iliwatoa Thomas Madimba na Edger Manake na kuwaingiza Mahlatse Maake na Karabo Tshepe na dakika ya 59, Domayo aliifungia Yanga bao la pili kwa shuti dhaifu ndani ya boksi baada ya mgongeo mzuri wa Msuva na Niyonzima.
Dakika ya 64, Tegete ambaye mashabiki wamempachika jina la Mturuki kutokana na kung’ara katika ziara ya hivi karibuni nchini humo  akiifungia mabao mawili katika mechi mbili tofauti, aliifungia Yanga bao la tatu akimalizia krosi ya Msuva na kuamsha shngwe za mashabiki.
Kutokana na kuonesha kiwango cha kuvutia, Tegete alishangiliwa kwa muda wote wa mchezo huo wa jana hadi pale alipotoka kumpisha George Banda na Dakika ya 88, Leopards walipata bao la pili kwa mkwaju wa penalti likifungwa na Ramagalela baada ya nyota huyo kuangushwa na Juma Abdul.
Yanga:Ali Mustafa ‘Barthez’, Mbuyu Twite, Oscar Joshua, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kelvin Yondan, Athuman Iddy ‘Chuji’, KAbange Twite, Frank Domayo, Jerry Tegete ‘Mturuki’, Didier Kavumbagu na Haruna Niyonzima
Leopards: Ayanda Mishali, Ernort Dzaga, Nkosiyabo Xakane, Harry Nyirenda, Humphrey Khoza, Munganga Djunga Jean, Mongezi Bobe, Thoimas Madimba, Abbas Amidu, Edger Manaka na Rodney Ramagalela

Comments