WAKATI Kamati
ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF)
chini Mwenyekiti wake Alex Mgongolwa ikimwidhinisha kipa Shaban Kado kuidakia Coastal
Union ya Tanga, Yanga watamkosa kiungo Kabange Twite katika raundi ya pili ya
Ligi Kuu itakayoanza Jumamosi hii.
Kabange ambaye ni pacha wa beki wa Mbuyu Twite katika
kikosi cha Yanga, alisajiliwa Januari kutoka
FC Lupopo ya DR Congo, lakini hayumo kwenye orodha ya nyota waliosajiliwa dirisha
dogo la usajili iliyotolewa jana na TFF.
Awali, TFF
ilimzuia Kabange Twite kuichezea Yanga hadi pale suala lake litakapoamuliwa
na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), baada ya Yanga kushindwa kupata
idhini ya FC Lupopo ya kumsajili nyota huyo, hivyo Fifa ndio walipasa kutoa
idhini.
Viongozi
wa Yanga kwa upande wao waliwasiliano na Lupopo kwa njia ya Kompyuta (TMS)
masaa mawili kabla ya usajili wa dirisha dogo kufungwa Desemba 15, lakini
hawakupata majibu, hivyo suala hilo
kuendelea kubaki mikononi mwa Fifa chini ya Kamati ya Haki na Uhamisho
Wachezaji.
Comments
Post a Comment