Pamoja na kufungwa na timu hiyo inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza , iitwayo Bank Asya 1. Lig, ambayo msimu uliopita
ilimaliza katika nafasi ya 10, Yanga ilicheza soka ya kuvutia.
Denizlispor Football iliyoanzishwa mwaka 1966, inatumia
Uwanja wenye kuingiza mashabiki 19,500 wa Denzili Ataturk na mafanikio yake
makubwa hivi karibuni ilikuwa mwaka 2002 waliposhika nafasi ya tano katika Ligi
Kuu ya nchini humo na kufuzu kwenye mchujo wa Kombe la UEFA.
Mwaka huo, ilifanya maajabu kwa kuzifunga timu zenye majina Ulaya
kama FC Lorient , Sparta Prague na Olympique Lyonnais , kabla ya kufungwa katika Raundi ya Nne na FC Porto ya Ureno, ambao walitwaa ubingwa wa michuano hiyo
mwishowe.
Katika mchezo wake wa kwanza wa kujipima nguvu, Yanga
ilitoka 1-1 na DSC Arminia Bielefeld
ya Ujerumani, bao la timu hiyo ya Jangwani likifungwa na Tegete.
Kikosi cha Yanga leo kilikuwa; Ally Mustafa ‘Barthez’, Juma
Abdu, Kabange Twite, Kevin Yondan, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Athumani Iddi
‘Chuji’, Haruna Niyonzima, Nurdin Bakari, Jerry Tegete/Didier Kavumbangu, Said
Bahanuzi/Hamisi Kiiza na Simon Msuva.
Comments
Post a Comment