Timu ya Taifa (Taifa Stars) itacheza mechi ya kujipima nguvu
dhidi ya Ethiopia .
Mechi hiyo itachezwa Januari 11 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Stars chini ya Kocha Mkuu Kim Poulsen inatarajia kuingia
kambini jijini Dar es Salaam
keshokutwa (Januari 6 mwaka huu) kujiandaa kwa mechi hiyo. Mechi hiyo itakuwa
kipimo cha mwisho kwa Ethiopia
kabla ya kwenda Afrika Kusini kwenye fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika
(AFCON) zitakazoanza Januari 19 mwaka huu.
Katika mechi yake ya mwisho, Taifa Stars iliifunga Zambia bao 1-0 katika mchezo wa kirafiki
uliofanyika Desemba 22 mwaka jana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam .
Mechi hiyo ya kirafiki dhidi ya Ethiopia
ni sehemu ya maandalizi ya mechi ya mchujo dhidi ya Morocco kuwania tiketi ya kucheza
fainali za Kombe la Dunia 2014. Mechi hiyo itachezwa Machi mwaka huu.
Wachezaji wanaotakiwa kambini ni Juma Kaseja kutoka Simba
ambaye pia ndiye nahodha wa Stars, Aishi Manula na Mwadini Ally wote kutoka
Azam. Mabeki ni Aggrey Morris (Azam), Amir Maftah (Simba), Erasto Nyoni (Azam),
Issa Rashid (Mtibwa Sugar), Kelvin Yondani (Yanga), Nadir Haroub (Yanga) na
Shomari Kapombe (Simba).
Viungo ni Salum Abubakar (Azam), Athuman Idd (Yanga), Amri
Kiemba (Simba), Khamis Mcha (Azam), Frank Domayo (Yanga), Mwinyi Kazimoto
(Simba) na Shabani Nditi (Mtibwa Sugar).
Washambuliaji ni John Bocco (Azam), Mbwana Samata (TP
Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Mrisho Ngasa (Simba), Simon
Msuva (Yanga), na Thomas Ulimwengu wa TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya
Congo (DRC).
Wakati benchi la Ufundi lina Kim, Sylvester Marsh (Kocha
Msaidizi), Juma Pondamali (Kocha wa makipa), Leopold Tasso (Meneja), Dk.
Mwanandi Mwankemwa (Daktari wa timu), Frank Mhonda (Mtaalamu wa tibamaungo) na
Alfred Chimela (Mtunza vifaa).
Comments
Post a Comment